Author: Admin

Klabu ya Azam FC imetangaza rasmi kukamilisha usajili wa mshambuliaji chipukizi, Aimar Hafidh Abubakar, maarufu kama ‘Haaland’, akitokea klabu ya Mlandege FC ya Zanzibar katika dirisha hili la usajili la Januari 2026. Usajili wa mchezaji huyo, ambaye amejizolea umaarufu kutokana na uwezo wake wa kufumania nyavu, unatajwa kuwa ni sehemu ya mkakati wa “Tajiri wa Jiji” kuimarisha safu yao ya ushambuliaji baada ya kufanya vizuri na kuiondosha Simba SC katika michuano ya Kombe la Mapinduzi. Kwa kuingia kwa Aimar Hafidh, Azam FC inaendeleza falsafa yake ya kusaka vipaji bora kutoka kanda ya Afrika Mashariki.

Read More

Nimeona baadhi ya mashabiki wa kandanda wakimtupia maneno ya kejeli beki wa kimataifa wa Ivory Karaboue Chamou anayeichezea klabu ya Simba kwa sasa. Mashabiki wengi wanamfuata na kumzodoa beki huyo kwenye mitandao ya kijamii mara baada ya Simba kupoteza mchezo wowote. Haya yote sababu yake nini? Na kwanini inakuwa hivyo. Kiufundi Karaboue Chamou ni beki mwenye nidhamu ya hali ya juu katika uchezaji wake. Ni beki tafu sana kama utaamua kwenda nae hewani au kufanya naye battle. Namkumbuka Karaboue Chamou aliyeifikisha Simba Hatua ya fainali ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika msimu uliopita mara baada ya Che Malone Fondoh kuumia…

Read More

KIKOSI cha Simba SC kimeanza rasmi maandalizi yake leo  Jumapili, Januari 11, 2026 uwanja wa Mo Simba Arena, kikielekeza nguvu kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Esperance de Tunis. Hatua hiyo inakuja baada ya mapumziko mafupi, huku benchi la ufundi likilenga kurejesha ushindani na umakini wa wachezaji kabla ya mechi hizo mbili muhimu. Mchezo wa kwanza wa hatua hiyo unatarajiwa kuchezwa Januari 24, 2026, ambapo Simba itakuwa ugenini nchini Tunisia. Mechi hiyo inatajwa kuwa ngumu kutokana na uzoefu na rekodi ya Esperance katika michuano ya kimataifa, jambo linalowafanya Wekundu wa Msimbazi kujiandaa kwa umakini mkubwa. Katika mazoezi…

Read More

Baada ya klabu ya Simba SC kuondoshwa katika michuano ya Kombe la Mapinduzi kufuatia kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa Azam FC, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa klabu hiyo, Ahmed Ally, ametoa kauli nzito ya kuwafariji mashabiki kupitia ujumbe wake wa, “Timu yangu, roho yangu, furaha yangu, maisha yangu wakati wote na nyakati zote,” akisisitiza kuwa mapenzi yake kwa klabu hiyo hayategemei matokeo ya muda mfupi bali ni ya kudumu. Kauli hiyo imetumika kama mkakati wa kupoza machungu ya mashabiki wa Msimbazi katika kipindi hiki kigumu cha Januari 2026, huku ikilenga kurejesha umoja na utulivu kikosini. Ahmed Ally amedhihirisha…

Read More

Dereva wa Anthony Joshua ameshtakiwa baada ya ajali nchini Nigeria ambayo ilimjeruhi bondia huyo na kuwaua marafiki zake wawili wa karibu, polisi wamesema. Adeniyi Mobolaji Kayode, mwenye umri wa miaka 46, alishtakiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Sagamu Ijumaa (Januari 2). Waendesha mashtaka wamemshtaki Bw. Kayode kwa kusababisha kifo kwa kuendesha gari mwendo wa hatari, kuendesha gari kwa uzembe , kuendesha gari bila uangalifu unaofaa, na kuendesha gari bila leseni halali ya udereva. Kesi hiyo imeahirishwa hadi Januari 20 Bondia huyo alipelekwa hospitalini Jumatatu baada ya kuokolewa kutoka kwenye mabaki ya ajali ya gari nchini Nigeria ambapo wawili walifariki.…

Read More

Swali Langu La Msingi Kuhusu Chama Clatous na Henoc Inonga Bacca Kuhusishwa Kutaka Kurejea Simba Sports ni hili hapa..✍️ Je zile Sababu ambazo zilipelekea Simba Sports wakaachana nao sasa hivi zitakuwa hazipo tena?? Manake yamezungumzwa Mengi sana wakati hawa wachezaji wanaondoka Simba.Kuna nyakati Mpaka Simba Sports wenyewe waliwasimamisha. Nauliza tena hizi Sababu sasa hivi hazipo tena Mpaka Kutaka Kurejea Simba Sports au ni Kitu gani? Ameandika mchambuzi wa michezo Wilson John Oruma (Mzee wa Jambia)

Read More

KOCHA wa Klabu ya Simba, Steve Barker, amesema kuwa mchezo wa kesho dhidi ya Muembe Makumbi katika Kombe la Mapinduzi ni muhimu kwa maandalizi ya kikosi chake. Amesema  licha ya kuelewa kuwa mashindano hayo yana uzito mkubwa kama ilivyo kwa mashindano ya kimataifa yanayowakabili baadaye. Barker amesema lengo kubwa la Simba katika michuano hiyo ni kuwapa wachezaji muda wa kucheza na kurejesha ubora wao wa ushindani baada ya mapumziko, huku akitumia fursa hiyo kujaribu mbinu mbalimbali kabla ya mechi ngumu zijazo. Barker ameongeza  kuwa ingawa Kombe la Mapinduzi  kipaumbele kikubwa kwa Simba, bado anaamini ni jukwaa zuri la kuwakagua wachezaji…

Read More

MENEJA wa timu ya Simba, Patrick Rweyemamu amesema hakuna sababu ya wapinzani kuwachukulia poa Wekundu wa Msimbazi licha ya kwenda Visiwani Zanzibar. Amesema  kikosi chenye wachezaji pungufu,  timu hiyo imejipanga kuonyesha ubora wake katika michuano ya Kombe la Mapinduzi. Simba kwa sasa wapo Visiwani Zanzibar tayari kwa ajili ya kushiriki michuano hiyo ya kihistoria, ambapo wanatarajiwa kushuka dimbani kesho Januari 3 kucheza mchezo wao wa kwanza dhidi ya Muembe Makumbi City, New Amaan Complex. Rweyemamu amesema licha ya kikosi hicho kuwa na mchanganyiko wa wachezaji wa kikosi cha kwanza na chipukizi kutoka timu ya vijana, dhamira ya Simba imebaki ileile…

Read More

TETESI za kiungo wa Singida Black Stars, Clatous Chama, kurejea tena ndani ya kikosi cha Simba SC zimezidi kupamba moto, baada ya mchezaji huyo kutoa kauli fupi iliyozua mjadala mkubwa miongoni mwa mashabiki wa Wekundu wa Msimbazi. Chama aliibua hisia hizo kupitia majibu yake kwa shabiki mmoja aliyemkaribisha kurejea Simba, ambapo mchezaji huyo alijibu kwa maneno mawili tu, “Mapema tu”, kauli ambayo wengi wameitafsiri kama ishara ya wazi ya uwezekano wa kurejea kwake Msimbazi. Katika kipindi hiki cha dirisha dogo la usajili, jina la Chama limekuwa likihusishwa kwa nguvu na Simba, huku ikielezwa kuwa mabingwa hao wa zamani wa Ligi…

Read More

Mshambuliaji wa Japani Kazuyoshi Miura, mchezaji mzee zaidi wa mpira wa miguu duniani, amesaini mkataba wa mwaka mmoja na klabu ya Ligi Daraja la Tatu ya Fukushima United FC. Miura bado anaendelea vizuri akiwa na umri wa miaka 58 na anatarajiwa kuanza mkopo wake wa nne katika miaka mingi akitokea klabu ya Yokohama FC. Atatimiza miaka 59 mwezi Februari, mwezi mmoja tangu aanze kutumikia timu hiyo ya Fukushima. Akijulikana kama “King Kazu” huko Japani, Miura pia amefurahia maisha ya soka Australia na Ulaya katika taaluma yake akichezea Genoa na Dinamo Zagreb. Alianza kusakata kabumbu Santos na kisha Palmeiras katika Serie…

Read More

Klabu ya Singida Black Stars itacheza mchezo rasmi wa ufunguzi wa michuano ya Mapinduzi Cup dhidi ya Mlandege siku ya leo katika dimba la New Amaan majira ya saa 10:15 jioni. Singida Black Stars tayari imewasili visiwani Zanzibar siku ya jana na kufanya mazoezi ya kurejesha utimamu wa miili ya wachezaji ili kujiweka sawa kuelekea mtanange huo. “Singida Black Stars tumepata heshima kubwa kucheza mechi ya kwanza ya uzinduzi wa Kombe la Mapinduzi 2026” Amesema Meneja Habari na Mawasiliano wa timu hiyo – @massanzajr

Read More

Mke wa zamani wa nyota wa PSG, Achraf Hakimi, Hiba Abouk, amedaiwa kuomba msamaha na kueleza kuzungushwa na majuto kwa kuomba talaka. Vyanzo vya karibu vinavyomfahamu mwanamitindo huyo wa Hispania vinadai kwamba Abouk alitenda kwa mihemko baada ya kuathiriwa na marafiki wake, na sasa anamuomba Hakimi amrudie. Hata hivyo, hali hii imeibua mashaka miongoni mwa mashabiki na wanasiasa wa mitandao, wengi wakisema kuwa matamshi ya Hiba yanaweza kuwa na mpango wake wa kisiasa au kifedha dhidi ya Hakimi. Wazo hili linatokana na habari mpya kuwa PSG imeongeza mkataba wa Hakimi, na kuongeza mshahara wake kutoka pauni milioni 10 hadi milioni 28 kwa mwaka, jambo ambalo linaweza kuathiri mgogoro…

Read More

Manchester United wanaripotiwa kujaribu kumrejesha James Garner Old Trafford ikiwa ni miaka mitatu tu baada ya kumuuza Everton. Kikosi cha Amorim kimekuwa na uhitaji wa kiungo mpya na nyota huyo ameonekna kuwa chaguo namba moja na la bei nafuu kuelekea dirisha la usajili la Januari. Miaka mitatu iliyopita Man United walimuuza Garner kwa Everton kwa pauni milioni 9 ambapo mkataba wake na klabu hiyo utamalizika msimu ujao wa joto.

Read More

Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Paul Makonda amesema amepigiwa simu na Watanzania mbalimbali ambao wameahidi kutoa Shilingi Milioni 100 kwa kila goli watakalofunga Taifa Stars siku ya leo dhidi ya Uganda na ile ya Tunisia Desemba 30 katika mashindano ya Afcon yanayoendelea nchini Moroco. Makonda amesema hayo alipokuwa akizungumza na wachezaji na benchi la ufundi la Stars kuelekea mchezo wao dhidi ya Uganda utakaochezwa siku ya leo katika dimba la Al Madina majira ya saa 2;30 usiku. “Kuwathibitisha kuwa Watanzania wako pamoja na nyinyi, juzi na jana nimepokea simu za Watanzania ninaowaamini na kuwaheshimu wameniambia nenda kawaambia…

Read More

Mshambuliaji wa Liverpool Alexander Isak anatarajiwa kukaa nje kwa angalau miezi miwili baada ya kuvunjika mguu na kufanyiwa upasuaji, meneja wa klabu hiyo ya Ligi Kuu nchini Uingereza, Arne Slot, alisema Jumanne. Isak alipata jeraha hilo alipoifungia Liverpool bao la kwanza katika ushindi wa 2-1 dhidi ya Tottenham Hotspur Jumamosi wakati mguu wake ulipokwama kati ya miguu ya Micky van de Ven huku mlinzi huyo akipiga mbizi kuzuia shuti lake. Jeraha hilo ni pigo kubwa kwa Liverpool wanapotafuta kuokoa utetezi wao wa ubingwa. “Itakuwa jeraha refu kwa miezi miwili. Hilo ni jambo la kusikitisha sana kwake na matokeo yake, kwetu…

Read More

Timu ya taifa Tanzania ‘Taifa Stars’ leo itamkosa Kiungo wake tegemezi Feisal Salum ‘Feitoto’ baada ya kupata kadi za njano kwenye michezo ya mwisho ya Taifa Stars kuwania kufuzu makala haya ya Kombe la mataifa Afrika AFCON 2025. Feitoto alipata kadi za njano kwenye mechi dhidi ya Guinea na DR Congo.

Read More

Wachezaji wa Manchester City watakuwa na siku tatu nje ya uwanja ili kufurahia likizo ya Krismasi lakini meneja Pep Guardiola anasema yeyote atakayefanya makosa ya kiwango cha juu wakati wa kurudi kwao hatacheza dhidi ya Nottingham Forest Jumamosi. “Kila mchezaji ana uzito. Wanarudi tarehe 25 na nitakuwepo kudhibiti ni kilo ngapi zinazoongezeka, (ili kuona kama) zina mafuta,” alisema Guardiola, ambaye anajulikana kwa kuwa mkali kuhusu lishe na urekebishaji. Mara tu wanapofika baada ya siku tatu nataka kuona watakavyorudi. Wanaweza kula lakini nataka kuwadhibiti. Lazima nifanye uteuzi wa (Desemba) 27 dhidi ya Nottingham Forest. Hebu fikiria mchezaji mmoja na sasa yuko…

Read More

Nigeria vs Tanzania ni mchezo mkali unaosubiriwa kwa shauku kwenye mashindano ya AFCON 2025 ikiwa ni hatua ya makundi nchini Morocco. Tayari mchezo wa ufunguzi ulishachezwa rasmi Desemba 21 ya Jumapili na wenyeji Morocco wakiibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Comoros. Leo ni kazi ya wawakilishi kutoka Tanzania, Taifa Stars wakiongozwa na nahodha Mbwana Samatta ambaye yupo nchini Morocco. Ni Nigeria vs Tanzania miongoni mwa kazi ngumu kwa wababe wote wawili ikiwa ni hatua ya makundi. Miguel Gamondi anatarajiwa kuchanga karata yake ya kwanza leo katika kampeni ya kuwania kufuzu hatua ya robo fainali. Jumanne, Desemba 23, 2025…

Read More

Matokeo ya Form Two 2025/2026 (Matokeo Kidato Cha Pili) NECTA FTNA Results 2025/2026 kwa Mikoa Yote na Wilaya Matokeo ya Form Two 2025/2026, yanayojulikana pia kama Matokeo ya Kidato Cha Pili au FTNA Results 2025/2026, ni miongoni mwa taarifa muhimu zaidi kwa wanafunzi, wazazi na walimu nchini Tanzania. Matokeo haya hutolewa na Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) na huonyesha tathmini ya kitaaluma ya wanafunzi waliomaliza mwaka wa pili wa elimu ya sekondari. Kupitia makala hii, utapata maelezo ya kina kuhusu Matokeo ya Kidato Cha Pili 2025/2026, umuhimu wake, hali ya sasa ya matokeo, mfumo wa madaraja, jinsi ya kuyaangalia,…

Read More

Ni nchi gani iliyoshinda Afcon 2024? Ivory Coast imeibuka mshindi wa Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2024 baada ya ushindi wa kusisimua dhidi ya timu ya taifa ya Nigeria katika mchezo wa fainali uliofanyika Uwanja wa Alassane Ouattara mjini Abidjan. Katika mchezo wa fainali uliochezwa Februari 11, 2024, Ivory Coast ilishinda kwa goli 2-1 dhidi ya Nigeria. Bao la ushindi lilifungwa na Sébastien Haller dakika ya 81, akimalizia shambulio kali la timu yake na kuipa Ivory Coast taji hili muhimu. Bao la kwanza la mchezo liliwekwa kimiani na William Troost-Ekong wa Nigeria, lakini Ivory Coast ilizirejesha pigo kupitia bao…

Read More