Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » SIMBA RASMI YAREJEA KAMBINI KUJIANDAA, MIPANGO NI MIKUBWA SASA
    KITAIFA

    SIMBA RASMI YAREJEA KAMBINI KUJIANDAA, MIPANGO NI MIKUBWA SASA

    By AdminJanuary 11, 2026No Comments2 Mins Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    simba
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    KIKOSI cha Simba SC kimeanza rasmi maandalizi yake leo  Jumapili, Januari 11, 2026 uwanja wa Mo Simba Arena, kikielekeza nguvu kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Esperance de Tunis.

    Hatua hiyo inakuja baada ya mapumziko mafupi, huku benchi la ufundi likilenga kurejesha ushindani na umakini wa wachezaji kabla ya mechi hizo mbili muhimu.

    Mchezo wa kwanza wa hatua hiyo unatarajiwa kuchezwa Januari 24, 2026, ambapo Simba itakuwa ugenini nchini Tunisia.

    Mechi hiyo inatajwa kuwa ngumu kutokana na uzoefu na rekodi ya Esperance katika michuano ya kimataifa, jambo linalowafanya Wekundu wa Msimbazi kujiandaa kwa umakini mkubwa.

    Katika mazoezi hayo, kocha Steve Barker na wasaidizi wake wanatarajiwa kuweka mkazo kwenye uimara wa safu ya ulinzi, kasi ya mashambulizi na matumizi sahihi ya nafasi.

    Lengo ni kuhakikisha kikosi kinakuwa imara kimwili na kiakili kabla ya safari ya kuelekea Tunis.

    Baada ya mechi ya kwanza, Simba itarejea nyumbani kujiandaa na mchezo wa marudiano utakaochezwa Januari 30, 2026, Benjamini Mkapa, Dar es Salaam.

    Uwanja wa nyumbani unatajwa kuwa silaha muhimu kwa Simba, huku mashabiki wakitarajiwa kujitokeza kwa wingi kuisukuma timu yao.

    Viongozi wa klabu wameeleza imani yao kwa kikosi walichonacho, wakisisitiza kuwa maandalizi ya mapema ni sehemu ya mkakati wa kufikia malengo makubwa msimu huu.

    Wamewataka wachezaji kuonyesha nidhamu, kujituma na kupigania nembo ya klabu uwanjani.

    Kurejea kwa Simba mazoezini ni ishara ya dhamira yao ya kufanya vizuri katika michezo ya Ligi ya MabingwaAfrika huku  Mashabiki wanasubiri kwa hamu kuona matokeo ya maandalizi hayo, wakitarajia timu yao kupigana kwa nguvu na kuandika historia mpya barani Afrika.

    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleAHMED ALLY ASEMA SIMBA NDIO MAISHA YANGU
    Next Article CHAMOU NI BEKI MZURI SANA WATU MSIMBEZE

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.