Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » Msiichukulie Poa Simba ya Sasa, Mazito Yatajwa
    KITAIFA

    Msiichukulie Poa Simba ya Sasa, Mazito Yatajwa

    By AdminJanuary 2, 2026No Comments2 Mins Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    simba
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    MENEJA wa timu ya Simba, Patrick Rweyemamu amesema hakuna sababu ya wapinzani kuwachukulia poa Wekundu wa Msimbazi licha ya kwenda Visiwani Zanzibar.

    Amesema  kikosi chenye wachezaji pungufu,  timu hiyo imejipanga kuonyesha ubora wake katika michuano ya Kombe la Mapinduzi.

    Simba kwa sasa wapo Visiwani Zanzibar tayari kwa ajili ya kushiriki michuano hiyo ya kihistoria, ambapo wanatarajiwa kushuka dimbani kesho Januari 3 kucheza mchezo wao wa kwanza dhidi ya Muembe Makumbi City, New Amaan Complex.

    Rweyemamu amesema licha ya kikosi hicho kuwa na mchanganyiko wa wachezaji wa kikosi cha kwanza na chipukizi kutoka timu ya vijana, dhamira ya Simba imebaki ileile ya kushindana kwa nguvu zote na kupambania matokeo chanya katika kila mchezo.

    Ameeleza kuwa baadhi ya wachezaji wao muhimu hawakuwepo kutokana na majukumu ya timu ya Taifa, lakini hilo halijapunguza ari ya kikosi, kwani maandalizi yamefanyika kwa umakini mkubwa kuhakikisha wanatimiza malengo yao.

    “Hatujaja na kikosi kamili kwa sababu wachezaji wengi wapo kwenye timu ya Taifa, lakini tumepanga vizuri na tumekuja kuonyesha kuwa tunahitaji kulichukua kombe hili,” alisema Rweyemamu.

    Meneja huyo ameongeza kuwa timu imeweka mikakati madhubuti kuhakikisha inafikia malengo yake, ikiwemo kupambana kwa nidhamu, kujituma uwanjani na kulinda heshima ya klabu katika mashindano hayo.

    Amesisitiza pia kuwa michuano hiyo ni fursa muhimu kwa kocha mpya wa Simba, Steve Barker, kupata nafasi ya kuliona na kulitathmini kikosi chake kwa karibu, jambo litakalompa mwanga wa kiufundi kuelekea changamoto zijazo za msimu.

    Simba SC
    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleRasmi Clatous Chama Atibitisha Kurejea Simba
    Next Article Kocha wa Simba Ahaidi Makubwa, Kazi Inaanza Mapinduzi Cup

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.