Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » Iran Yatangaza Huenda Isishiriki Kombe la Dunia 2026
    KIMATAIFA

    Iran Yatangaza Huenda Isishiriki Kombe la Dunia 2026

    By AdminMarch 12, 2026No Comments2 Mins Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    Waziri wa Michezo na Vijana wa Iran, Ahmad Donyamali, amesema timu ya taifa ya wanaume ya nchi hiyo huenda isishiriki katika michuano ya FIFA World Cup 2026 kutokana na hali ya usalama na mvutano wa kisiasa unaoendelea.

    Akizungumza katika mahojiano na kituo cha televisheni cha michezo cha Islamic Republic of Iran Broadcasting (IRIB) siku ya Jumanne, Donyamali alisema mazingira ya sasa hayaruhusu Iran kushiriki katika mashindano hayo makubwa ya soka duniani.

    “Kwa kuzingatia kwamba serikali hii imehusika katika kumuua kiongozi wetu, hatuna kabisa mazingira sahihi ya kushiriki Kombe la Dunia. Wachezaji wetu hawako salama, na hali iliyopo hairuhusu ushiriki,” alisema.

    Aliongeza kuwa katika miezi nane hadi tisa iliyopita, Iran imekumbwa na vita viwili ambavyo vimesababisha vifo vya maelfu ya raia wake, hali ambayo imeathiri kwa kiasi kikubwa shughuli nyingi za taifa hilo ikiwemo michezo.

    Wakati huo huo, Rais wa Shirikisho la Soka la Iran, Mehdi Taj, naye alihoji uwezekano wa timu ya taifa kushiriki michuano hiyo, akitaja changamoto zinazowakabili wachezaji hasa upande wa wanawake.

    Taj alitoa kauli hiyo baada ya wachezaji sita wa timu ya taifa ya wanawake ya Iran kupewa visa za kibinadamu na Australia kufuatia kushiriki michezo nchini humo. Alisema iwapo hali ya sasa itaendelea kuwa hivyo, itakuwa vigumu kwa Iran kutuma timu yake katika mashindano yatakayofanyika Marekani.

    Kauli hizo zimeibua mjadala mkubwa kuhusu mustakabali wa ushiriki wa Iran katika FIFA World Cup 2026, wakati mvutano wa kisiasa na kiusalama ukiendelea katika eneo la Mashariki ya Kati.

    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleMukwala Hakuna wa Kumzuia Libya, Gari Limewaka Hatari
    Next Article Ubabe wa Yanga Ndani Wazidi Kuonekana Msimu wa 2025/26

    Related Posts

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    March 18, 2026

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    March 18, 2026

    Drone Yashambulia Tangi la Mafuta Karibu na Uwanja wa Ndege wa Dubai.

    March 16, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    Makocha wa Simba na Yanga Wagawana Tuzo za Mwezi Februari

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.