Mamlaka za Dubai zimesema kwamba moto umeteketeza eneo la karibu na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dubai baada ya shambulio la kutumia drone kugonga tangi la mafuta karibu na Uwanja huo wa Ndege. 
Moto ulizuka baada ya drone kushambulia na kugonga tangi la kuhifadhia mafuta, jambo lililosababisha moto mkubwa katika eneo hilo. 
Shambulio hili lilihusiana na mzozo unaoendelea wa kijeshi katika eneo la Mashariki ya Kati. 
Timu za Zimamoto na Uokoaji za Dubai zinashughulikia tukio hilo na juhudi zinaendelea ili kudhibiti moto huo.
Mamlaka zimekuwa zikichukua hatua zote muhimu kuhakikisha usalama kwa watu katika eneo hilo. 
Ripoti za awali zinasema hakuna mtu aliyepata majeraha hadi sasa kutokana na tukio hili. 
Mamlaka ya Anga ya Dubai imesema shughuli za baadhi ya Ndege zilisimama kutua au kuingia katika uwanja wa ndege kwa muda.
