Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » TAKWIMU ZA KELVIN JOHN HUKO DENMARK
    KIMATAIFA

    TAKWIMU ZA KELVIN JOHN HUKO DENMARK

    By AdminSeptember 29, 2025No Comments1 Min Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    kelvin john
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    Mshambuliaji wa AaB Fodbold ya Denmark, Kelvin John licha ya timu yake hiyo kupoteza kwa mabao 2-1 dhidi ya Lyngby Boldklub amezidi kuwa bora na amesema huu ni msimu wake wa kuonyesha kiwango bora.

    Juzi, timu ya Mtanzania huyo ilipoteza mabao 2-1 dhidi ya Lyngby Boldklub kwenye muendelezo wa Ligi Daraja la Kwanza Denmark na licha ya kufungwa, John alionyesha kiwango bora kwa kufunga bao moja ambalo linamfanya kuwania tuzo ya mchezaji bora wa mechi, kura zinazopigwa na mashabiki.

    Bao alilofunga linamfanya kufikisha jumla ya mabao sita kwenye mechi 10 alizocheza. Timu hiyo ipo nafasi ya saba kwenye msimamo wa ligi baada ya kukusanya pointi 14.

    Akizungumza na AaB TV, John alisema huu ni msimu wake wa kufanya vizuri, kuonyesha kiwango bora na kuwa na muendelezo wa kufunga. “Ninapofunga kila mechi inanipa ujasiri wa kuendelea kufunga, hivyo huu ni msimu wangu wa kufanya vizuri na kuisaidia timu yangu imalize nafasi nzuri,” alisema John

    Huu ni msimu wa pili kwa John kuitumikia timu hiyo ambayo msimu uliopita ilimaliza mkiani mwa msimamo wa Ligi Kuu Denmark na kushushwa daraja, hivyo sasa inashiriki Ligi Daraja la Kwanza.

    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleUKWELI WA ISHU YA YANGA KUACHANA NA KOCHA FOLZ
    Next Article FIFA YAIADHIBU AFRIKA KUSINI KWA KUMCHEZESHA MCHEZAJI ASIYE NA SIFA

    Related Posts

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    March 18, 2026

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    March 18, 2026

    Drone Yashambulia Tangi la Mafuta Karibu na Uwanja wa Ndege wa Dubai.

    March 16, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.