Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home ยป NYOTA WA FOUNTAIN GATE ALAMBA MKATABA WA MIAKA 17
    KITAIFA

    NYOTA WA FOUNTAIN GATE ALAMBA MKATABA WA MIAKA 17

    By AdminJuly 27, 2025No Comments1 Min Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    TIMU ya Fountain Gate FC imemtambulisha mchezaji chipukizi Juma Issa Abushiri (Chuga) kutoka timu ya taifa ya vijana ya Tanzania (U-17). Nyota huyo amesaini mkataba wa miaka mitano kuwa kwenye timu hiyo ambayo ina uhakika wa kushiriki Ligi Kuu Tanzania Bara ya NBC ambayo ni namba nne kwa ubora msimu wa 2025/26.

    Akizungumza katika Hoteli ya Tanga Beach Resort jijini Tanga, baada ya kumsainisha mchezaji huyo, Rais wa Fountain Gate, Japhet Makau, amesema kuwa usajili huo ni sehemu ya kuendeleza utamaduni wa timu hiyo wa kuwapa nafasi vijana.

    Ameeleza kuwa Juma Issa ni zao la timu za vijana za Fountain Gate tangu akiwa mdogo, na alisoma katika shule za timu hiyo, ambako kipaji chake kiligunduliwa.

    Amesema kuwa lengo la kuwasajili vijana ni kuwapa fursa ya kuonesha ushindani katika Ligi Kuu na kufungua milango ya kucheza soka nje ya nchi.

    Aidha, katika msimu uliopita, timu hiyo ilipandisha vijana takriban wanane walio chini ya umri wa miaka 20, ambao wamepata nafasi ya kuonesha uwezo wao katika timu ya wakubwa.

    Ofisa Habari wa Fountain Gate, Issa Mbuzi ameweka wazi kuwa mpango mkubwa wa timu hiyo ni kufanya vizuri kwa msimu mpya na timu ambazo ziliwafunga hazitawafunga msimu mpya wa 2025/26.

    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleUSAJILI WA KWANZA SIMBA HUU HAPA, MSHAMBULIAJI WA MABAO KUTAMBULISHWA
    Next Article KIVUMBI LEO FAINALI YA WAFCON NIGERIA VS MOROCCO

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.