Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home ยป USAJILI WA KWANZA SIMBA HUU HAPA, MSHAMBULIAJI WA MABAO KUTAMBULISHWA
    KITAIFA

    USAJILI WA KWANZA SIMBA HUU HAPA, MSHAMBULIAJI WA MABAO KUTAMBULISHWA

    By AdminJuly 27, 2025No Comments1 Min Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    MSIMBAZI kumeanza kumechangamka kupitia usajili baada ya dirisha la usajili kufunguliwa huku wakiwa hajatangaza mchezaji hata mmoja mpya ambaye ameshasaini kandarasi Simba SC.

    Mabosi wa Singida Black Stars, wameeleza kuwa Jonathan Sowah ambaye ni mshambuliaji wao wameingia makubaliano ya kumuuza ndani ya Simba SC kwa makubaliano maalumu.

    Hivyo Sowah anakuwa nyota wa kwanza usajili wake kuwekwa wazi baada ya timu ya Simba SC kuwa kwenye sarakasi nyingi kutokana na wachezaji ambao walikuwa wanatajwa kuwa kwenye hesabu za Kocha Mkuu, Fadlu Davids kutambulishwa kwa timu pinzani ambayo ni Yanga SC.

    Miongoni mwa wachezaji ambao walikuwa wanatajwa kuwa kwenye hesabu za Simba SC wakatambulishwa Yanga SC ni kiungo Ballac Conte ambaye kasaini dili la miaka mitatu Jangwani.

    Imeelezwa Sowah anakuja kuchukua nafasi ya straika Lionel Ateba ambaye anatarajiwa kutimkia uarabuni. Imethibitishwa kuwa Simba walikamilisha dili la Sowah usiku wa kuamkia Jumatano Julai 16 2025.

    Ikumbukwe kwamba kwa msimu wa 2024/25 Sowah kwenye ligi ikiwa ni ingizo jipya katika dirisha dogo alifunga jumla ya mabao 13 akiwa na Singida Black Stars ambayo ilicheza fainali ya CRDB Federation Cup dhidi ya Yanga SC ikapishana na taji hilo.

    Simba SC
    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleRASMI: SIMBA SC IMEFIKIA MAKUBALIANO NA FEISAL
    Next Article NYOTA WA FOUNTAIN GATE ALAMBA MKATABA WA MIAKA 17

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.