Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » MOURINHO ATANGAZA VITA KALI DHIDI YA CHELSEA LEO
    KIMATAIFA

    MOURINHO ATANGAZA VITA KALI DHIDI YA CHELSEA LEO

    By AdminSeptember 30, 2025No Comments1 Min Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    Kocha Mkuu wa Benfica ya Ureno, Jose Mourinho, anarejea leo kwenye dimba la Stamford Bridge, uwanja wenye historia kubwa katika maisha yake ya soka. Safari hii anarejea kama mpinzani, akiiongoza Benfica kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya mabingwa wa dunia, Chelsea. Mourinho alitangazwa kuwa kocha mkuu wa Benfica wiki iliyopita na leo anakabiliwa na mtihani wake mkubwa wa kwanza akiwa na timu hiyo mpya.

    Akizungumza kuelekea mchezo huo, Mourinho alisema anajihisi kama yupo nyumbani lakini sasa anawakilisha Benfica na lengo lake ni moja tu — kushinda. “Najihisi kama niko nyumbani, lakini ndani ya dakika 90 sitafikiria nilikotoka. Mimi si ‘The Blues’ tena, mimi ni mwekundu wa Benfica na nataka kushinda,” alisema.

    Mourinho aliwahi kuinoa Chelsea katika vipindi viwili tofauti (2004–2007 na 2013–2015) na kuandika historia kwa kutwaa mataji makubwa ikiwemo ubingwa wa Ligi Kuu England mara tatu, Kombe la FA mara moja, Kombe la Ligi mara tatu na Ngao ya Jamii mara moja. Kurejea kwake Stamford Bridge leo ni tukio la kihistoria linaloleta kumbukumbu nyingi, huku dunia ya soka ikisubiri kuona kama “The Special One” ataandika ukurasa mwingine wa kukumbukwa.

    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleWAJUE WAPINZANI WA SIMBA MECHI INAYOFUATA CAF
    Next Article TETESI: NABI YUPO MBIONI KUIONA KLABU HII KUBWA NCHINI

    Related Posts

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    March 18, 2026

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    March 18, 2026

    Drone Yashambulia Tangi la Mafuta Karibu na Uwanja wa Ndege wa Dubai.

    March 16, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.