Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » MBEYA DAY NI LEO KUNOGESHWA NA MECHI KALI DHIDI YA AZAM FC
    KITAIFA

    MBEYA DAY NI LEO KUNOGESHWA NA MECHI KALI DHIDI YA AZAM FC

    By AdminSeptember 6, 2025No Comments2 Mins Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    PAZIA la Ligi Kuu Tanzania Bara ya NBC ambayo ni namba nne kwa ubora linakaribia kufunguliwa ikiwa ni siku zinahesabiki kwa kuwa Septemba 17 kazi inatarajiwa kuanza.

    Leo kuna tamasha kubwa nyanda za juu Kusini, ambapo Mbeya City iliyorejea kwa mara nyingine ndani ya Ligi Kuu Tanzania Bara ambayo ni namba nne kwa ubora Afrika watakuwa na jambo lao.

    Mbey City, The Purple Nation,  Uwanja wa Sokoine, Mbeya watafanya utambulisho wa kikosi chao cha msimu wa 2025/2026 unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa.

    Miongoni mwa wachezaji waliopo Mbeya City ni kipa wa zamani wa Simba SC na Yanga SC, Beno Kakolanya ambaye yupo hapo kwa mara nyingine tena katika kutimiza majukumu yake.

    Kutakuwa na mchezo mkali wa kirafiki kati ya wenyeji Mbeya City dhidi ya matajiri wa Dar, Azam FC ambao unatarajiwa kuchezwa Uwanja wa Sokoine, Mbeya.

    Kocha Msaidizi wa Mbeya City Mussa Rashid ameweka wazi kuwa wapo tayari kwa mchezo huo na watatoa burudani nzuri kwa mashabiki watakaojitokeza.

    Hasheem Ibwe, Ofisa Habari wa Azam FC ameweka wazi kuwa wapo tayari kwa mchezo na wapinzani wao Mbeya City wamefanya makosa kuichagua Azam FC kwa kuwa ina hasira kutafuta matokeo hata kama imealikwa.

    Mgeni rasmi kwenye tamasha hilo ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Beno Malisa atashuhudia burudani zote kwenye tukio hili kubwa.

    Azam FC
    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleMIKE TYSON KUZICHAPA NA FLOYD MAYWEATHER
    Next Article Barcelona, Liverpool na Madrid vitani kumgombea Marc Guehi

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.