Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » KWA MARA YA KWANZA MOROCCO YAANDIKA HISTORIA YA KUSSHINDA KOMBE LA DUNIA KWA VIJANA
    KIMATAIFA

    KWA MARA YA KWANZA MOROCCO YAANDIKA HISTORIA YA KUSSHINDA KOMBE LA DUNIA KWA VIJANA

    By AdminOctober 21, 2025No Comments1 Min Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Morocco
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    Timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 20 ya Morocco imeandika historia baada ya kutwaa taji la Kombe la Dunia la Vijana (FIFA U-20 World Cup) kwa mara ya kwanza, ikipata ushindi wa mabao 2–0 dhidi ya Argentina katika mchezo wa fainali uliopigwa Jumapili.

    Shujaa wa pambano hilo alikuwa mshambuliaji Yassir Zabiri, aliyetikisa nyavu mara mbili katika dakika ya 12 na 29, akiiongoza Morocco kutwaa ubingwa huo wa kihistoria. Ushindi huo umeifanya Morocco kuwa taifa la kwanza kutoka Afrika kushinda taji hilo tangu Ghana ilipofanikiwa mwaka 2009.

    Argentina, ambayo ilikuwa haijapoteza mchezo wowote hadi kufika fainali, ilikosa huduma ya nyota wake wawili muhimu Claudio Echeverri wa Bayer 04 Leverkusen na Franco Mastantuono wa Real Madrid CF — hali iliyochangia kuporomoka kwao katika mchezo wa mwisho.

    Safari ya Morocco kuelekea ubingwa ilikuwa ya kuvutia. Walimaliza hatua ya makundi wakiwa vinara baada ya kushinda dhidi ya Uhispania, Brazil na Mexico, kisha kuiondosha Korea Kusini katika hatua ya 16 bora, Marekani robo fainali, na Ufaransa nusu fainali kabla ya kuhitimisha kazi kwa kuivunja Argentina katika fainali.

    Post navigation

    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleAZAM FC YAJAWA MATUMAINI YA KUBADILISHA HISTORIA YA KIMATAIFA
    Next Article Ronaldo kumsogeza Lewandowski Al-Nassr

    Related Posts

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    March 18, 2026

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    March 18, 2026

    Drone Yashambulia Tangi la Mafuta Karibu na Uwanja wa Ndege wa Dubai.

    March 16, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.