Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » KIBU NAYE KUIPA ‘THANK YOU’ SIMBA?….WAMAREKANI WAZIDI KUDATA NAYE KILA SIKU
    KITAIFA

    KIBU NAYE KUIPA ‘THANK YOU’ SIMBA?….WAMAREKANI WAZIDI KUDATA NAYE KILA SIKU

    By AdminJuly 22, 2025No Comments2 Mins Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    kibu
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    NDOTO ya mshambuliaji wa Simba SC na Taifa Stars, Kibu Dennis kucheza soka la kulipwa Marekani inakaribia kutimia baada ya klabu ya Nashville kumwongezea wiki ya majaribio kutokana na kile kinachoelezwa ni kivutio kwa makocha wa kikosi hicho.

    Kwa mujibu wa taarifa kutoka vyanzo vya karibu na mchezaji huyo, Kibu ambaye yuko Marekani tangu mwisho wa mwezi Juni, alikuwa amepewa wiki mbili za awali za kuonyesha uwezo wake.

    Hata hivyo, baada ya kipindi hicho kukamilika, uongozi wa Nashville SC inayoshiriki Ligi Kuu Marekani umevutiwa na mwenendo wake na kuamua kumwongeza wiki nyingine ya tathmini ya kiufundi.

    “Kibu anapambana kweli kweli,” alisema mmoja wa watu wa karibu na nyota huyo aliyeko jijini Nashville.

    “Hapa soka siyo lelemama. Wachezaji wapo wengi, ushindani ni mkubwa. Lakini mpaka kumpa wiki ya tatu, ina maana ana kitu cha ziada.”

    Klabu hiyo inayoshika nafasi ya pili kwenye kundi la Mashariki katika Ligi Kuu ya Marekani, imekuwa na mpango wa kuimarisha kikosi chake hasa upande wa winga mwenye kasi na uwezo wa kucheza namba 7 na 11, ambayo Kibu anaweza kucheza kwa ufanisi mkubwa.

    Chanzo cha kuaminika kutoka Marekani, kilinukuliwa na gazeti la  Mwanaspoti: “Majaribio yanafanyika na kikosi cha pili (reserve team), lakini waamuzi ni benchi kuu la ufundi. Walianza na wachezaji watano, baada ya wiki mbili watatu walikatwa. Kibu na kijana mmoja kutoka Brazil ndio waliobaki na kuongezewa muda kwa sababu walionesha kitu.”

    Kwa upande mwingine, taarifa kutoka Simba SC zinaeleza, iwapo Kibu atafaulu majaribio hayo, Nashville SC italazimika kuwasilisha ofa rasmi ya kumnunua mchezaji huyo, ambaye bado ana mkataba na Wekundu wa Msimbazi hadi mwishoni mwa msimu ujao.

    Katika mazungumzo ya awali, kocha wa kikosi cha pili cha Nashville, Michael Nsien ambaye ni msaidizi wa kikosi cha kwanza alieleza kuvutiwa na ubora wa Kibu katika kupiga pasi, kasi, pamoja na uwezo wa kumiliki mpira katika presha.

    Hiyo ndiyo sababu inayoelezwa kumtazama kwa karibu zaidi.

    Mdau wa soka wa Tanzania anayeishi mjini Nashville, Abdallah Karim, amenukuliwa na gazeti la Mwanaspoti:

    “Waafrika wako wachache kwenye kikosi hiki. Kibu ana nafasi nzuri sana. Kama akijituma wiki hii, naamini anaweza kumsajili, hii timu ina uwezo mkubwa kifedha.”

    Simba SC
    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleHUYU HAPA KAPEWA MAJUKUMU YA USAJILI SIMBA SC, ASEMA MTULIE
    Next Article KOCHA WA MAMELOD SUNDOWN KUULA YANGA….JAMAA ANA MIAKA 34 TU

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.