Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home ยป JEAN AHOUA AINGIA KWENYE MTIHANI MWINGINE SIMBA
    KITAIFA

    JEAN AHOUA AINGIA KWENYE MTIHANI MWINGINE SIMBA

    By AdminSeptember 15, 2025No Comments2 Mins Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    JEAN Ahoua kiungo mshambuliaji namba moja wa Simba SC kwenye mtihani mwingine ndani ya kikosi hicho kinachonolewa na Kocha Mkuu, Fadlu Davids itakuwa Septemba 16 2025.

    Ahoua ni namba moja kwenye utengenezaji mipango ndani ya kikosi hicho, msimu wa 2024/25 alitengeneza jumla ya pasi 9 za mabao.

    Mbali na kutengeneza pasi hizo 9 za mabao alifunga jumla ya mabao 16 akiwa ni mshambuliaji namba moja kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara inayodhaminiwa na NBC.

    Katika pasi na mabao aliyofunga alikwama kufunga mbele ya watani zao wa jadi Yanga SC na alikwama kutengeneza pasi mbele ya watani zake hao jambo ambalo linamfanya awe kwenye mtihani mwingine kujibu maswali aliyokwama msimu uliopita.

    Kazi inatarajiwa kuanza Septemba 16 2025 kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii ambapo wababe hawa wawili wanatarajiwa kukutana.

    Vita yake kubwa ilikuwa na mwamba Pacome ambaye ni kiungo mshambuliaji wa Yanga SC huyu aliwapa dozi Simba SC walipokutana kwenye mchezo wa funga kazi Uwanja wa Mkapa mzunguko wa pili baada ya kufunga bao moja na kutoa pasi ya bao wakati ubao uliposoma Yanga SC 2-0 Simba SC.

    Ni siku moja imebaki kwa watani hawa kukutana uwanjani huku kila mmoja akivutia kwake kuhusu kuanza vema kwa kutwaa taji la Ngao ya Jamii.

    Ikumbukwe kwamba kwenye mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya Gor Mahia, Ahoua alianza kikosi cha kwanza na alifungua akaunti ya pasi za mabao alipompa Hamza dakika ya 7 na mwisho ubao wa Uwanja wa Mkapa Septemba 10 2025 ulisoma Simba SC 2-0 Gor Mahia.

    Simba SC
    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleZIMBWE JR AFIKIRIA MAKUBWA YANGA SC
    Next Article YAMEBAKI MASAA KUELEKEA DABI YA KARIAKOO

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.