Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » YANGA YAIJIBU TFF, DAWA YA DENI NI KULIPA KWA WAKATI
    KITAIFA

    YANGA YAIJIBU TFF, DAWA YA DENI NI KULIPA KWA WAKATI

    By AdminJune 11, 20251 Comment2 Mins Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    yanga
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    Klabu ya Yanga imejibu mapigo baada ya Shirikisho la soka Tanzania (TFF) kudai klabu hiyo fedha zao za zawadi katika mashindano mbalimbali zikatwe kulipia malipo wanayotakiwa kuilipa kwa TFF huku ikidai kuwa haijawahi kulipwa fedha yoyote ya Ubingwa wa Kombe la Shirikisho kwa Misimu mitatu mfululizo, (2021/2022, 2022/2023 na 2023/24).

    Taarifa ya Juni 10, 2025 iliyotolewa na klabu hiyo imeeleza taarifa ya TFF Madai hayo imeshindwa kufafanua deni lenyewe na kubainisha kuwa TFF wamekuwa wakishikila fedha hizi za Ubingwa kwenye akaunti zao kila Msimu unapomalizika huku wakifahamu ni makosa na ni kinyume cha utaratibu.

    Yanga Sc imesema hakuna uthibitisho wowote wa kimaandishi kuonyesha kama TFF wamewahi kulipa fedha hizo za Ubingwa kwa Klabu ya Yanga na na kusisitiza kuwa ni aibu na fedheha na kumtia dosari mdhamini kuendesha mashindano bila kumlipa Bingwa kwa misimu mitatu mfululizo.

    “Tunaelekeza, dawa ya deni ni kulipa kwa wakati ikiwa ni haki ya mshindi na inampa heshima mdhamini wa mashindano. leleweke, ada za malipo ya wachezaji wa kiger kigeni walizozisema kwenye taarifa yao hulipwa mwanzo wa msimu mpya na hela hizi za Ubingwa hutolewa Mwisho wa msimu.” — imesema taarifa ya Yanga Sc.

    “Klabu ya Young Africans haijawahi kupokea taarifa yoyote rasmi kutoka TFF kuhusu Klabu yetu kuwa na deni kwao. Uongozi wa Klabu ya Young Africans unaendelea kusisitiza kulipwa pesa yake ya Ubingwa wa Kombe la Shirikisho la CRDB, kwa msimu wa 2023/24 ili tuweze kucheza mchezo wa Fainali siku ya tarehe 28 Juni, 2025.” — imesema Yanga Sc

    Yanga SC
    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleBAADA YA KUONA FEI TOTO ANAWEZA KUSEPA…AZAM WAHAMISHA NGUVU KWA STAA WA SIMBA
    Next Article TFF YATANGAZA UCHAGUZI MKUU AGOSTI 16, 2025 JIJINI TANGA

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    View 1 Comment

    1 Comment

    1. muppu on June 12, 2025 08:29

      Pretty! This has been a really wonderful post. Many thanks for providing these details.

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.