Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » BAADA YA KUONA FEI TOTO ANAWEZA KUSEPA…AZAM WAHAMISHA NGUVU KWA STAA WA SIMBA
    KITAIFA

    BAADA YA KUONA FEI TOTO ANAWEZA KUSEPA…AZAM WAHAMISHA NGUVU KWA STAA WA SIMBA

    By AdminJune 9, 2025No Comments2 Mins Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    HAWAJAWEKA wazi lakini tafsiri ya kiufundi ni kwamba Azam FC wako kwenye harakati za kujiandaa na lolote kwenye nafasi ya Feisal Salum ‘Fei Toto’

    Staa huyo ambaye bado ana mkataba wa mwaka mmoja na Azam amekuwa akihusishwa na kujiunga na Simba, Yanga na Kaizer Chiefs msimu ujao ambapo kila mmoja kwa wakati wake anapambana kupata ahueni ya dau. Azam wamekuwa wakisisitiza kwamba mchezaji wao anauzwa kwa zaidi ya Sh1 bilioni.

    Ili kuziba pengo lake, Azam FC iko kwenye mazungumzo na Vipers ya Uganda kuhusu kiungo wake Allan Okelo  ambaye Simba pia iliwahi kumtaka, lakini ilijibiwa kwamba mchezaji huyo hauzwi.

    Hapo awali  kikosi hicho kilipiga hesabu kubwa za kumsajili kiungo mshambuliaji, Okello ambaye naye ni fundi wa mguu wa kushoto kama ilivyo Elie Mpanzu.

    SIMBA ILIFELI HAPA

    Wekundu hao wa Msimbazi walimtaka Okello, kama kiungo mshambuliaji kupitia dirisha dogo la usajili lililofunguliwa Desemba 15 mwaka jana.

    Utata kwa Simba kumpata Okello,ukawa kwa Rais wa klabu hiyo Lawrence Mulindwa, ambaye amekuwa mgumu kuachia mastaa wake muhimu wa kikosi hicho kuuzwa.

    Taarifa za ndani kutoka Uganda zilisema kuwa: “Tumeanza mazungumzo na Azam wakimhitaji Okello, hatujamalizana lakini ni mazungumzo pekee ambayo hatujafikia mwisho.

    “Unajua Okello anatakiwa na klabu nyingi, lakini hata sisi Vipers tunahesabu naye tutaona kipi tutafikia makubaliano kati yetu na Azam.”

    Vipers inashika nafasi ya kwanza katika ligi ya Uganda ikiwa imecheza mechi 30, ikishinda 21,sare sita na kupoteza mitatu,huku Azam ikiwa namba tatu katika msimamo ikisalia na mechi mbili mkononi kati ya 30, huku Okello akiwa amefunga mabao 19 ndani ya msimu mmoja ambao huu ni wa pili tangu alipoanza kuitumikia Vipers katika mashindano hayo.

    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleGIFT FRED: BEKI WA YANGA APATA DILI NONO
    Next Article YANGA YAIJIBU TFF, DAWA YA DENI NI KULIPA KWA WAKATI

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.