Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home ยป TETESI ZA SOKA LEO JUMANNE TAREHE 05-08-2025
    TETESI ZA SOKA

    TETESI ZA SOKA LEO JUMANNE TAREHE 05-08-2025

    By AdminAugust 5, 2025No Comments2 Mins Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    Mshambuliaji wa Slovenia kutoka RB Leipzig, Benjamin Sesko (22), anatumia mbinu za kisiasa katika usajili kwa kuzitumia Newcastle na Manchester United kuzipambanisha ili apate dili bora zaidi.

    Newcastle wameonyesha nia mpya ya kumsajili beki wa kati wa England, Marc Guehi, kwa ofa ya takriban pauni milioni 40, lakini Crystal Palace wanataka pauni milioni 50 ili kumuachia mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25.

    Kocha David Moyes anataka kufanya usajili wa hadi wachezaji sita zaidi kwa ajili ya Everton, ikiwa ni pamoja na viungo wa kati wawili na wachezaji wa pembeni wawili.

    Tottenham wameambiwa watalazimika kulipa euro milioni 30 (pauni milioni 26) ili kumsajili kiungo wa Hispania Marc Casado (21) kutoka Barcelona.

    Winga wa Brazil Rodrygo (24) anataka kubaki Real Madrid licha ya kuvutiwa na Tottenham, Arsenal na Liverpool.

    Crystal Palace wanakabiliana na ushindani kutoka Juventus katika harakati za kumsajili beki wa kulia wa Girona, Arnau Martinez (22) raia wa Hispania.

    Kiungo wa kati wa Napoli na Sweden, Jens Cajuste (25), anapendelea kurejea Ipswich Town kuliko kwenda Burnley au ligi ya Saudi Arabia.

    Stuttgart wanakaribia kufanikisha dili la kumsajili kiungo wa kati wa Ureno, Fabio Vieira (25), kutoka Arsenal.

    Porto walivutiwa na beki wa Poland Jakub Kiwior (25), lakini walikataa kutimiza thamani ya euro milioni 30 (pauni milioni 26) iliyowekwa na Arsenal.

    Tottenham wanatataka kumuuza kiungo wa kati kutoka Mali, Yves Bissouma (28), ili kutoa nafasi kwa Conor Gallagher, kiungo wa kati wa England mwenye umri wa miaka 25 kutoka Atletico Madrid.

    Liverpool wanafuatilia maendeleo ya beki wa Brentford na timu ya taifa ya Ireland, Nathan Collins (24).

    West Ham wamewasilisha ofa mpya ya pauni milioni 10 kwa Botafogo ili kumsajili kipa wa Kibrazil John Victor (29).

    Bayer Leverkusen wanamtaka mshambuliaji wa Denmark wa Manchester United, Rasmus Hojlund (22), lakini wanakumbana na ushindani kutoka AC Milan, Inter Milan na Juventus.

    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleSAMATTA KUCHEZA LIGI KUU YA UFARANSA
    Next Article RASMI: CLEMENT MZIZE KUUZWA KWA WAARABU TIMU HII

    Related Posts

    SIMBA MBONI KUMALIZANA NA BEKI HUYU WA KAZI KUTOKA AL HILAL

    January 11, 2026

    Rasmi Clatous Chama Atibitisha Kurejea Simba

    January 2, 2026

    Done Deal: Simba Wamuuza Jean Ahoua Milioni 300 Kwenda Raja Casablabca, Fadlu Asuka Mpango Mzima

    December 15, 2025
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.