Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home ยป Tanzania Yaiomba China Msaada Kukamilika Miundo Mbinu ya AFCON 2027
    KITAIFA

    Tanzania Yaiomba China Msaada Kukamilika Miundo Mbinu ya AFCON 2027

    By AdminFebruary 10, 2026No Comments1 Min Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Tanzania
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    Serikali ya Tanzania imeiomba Jamhuri ya Watu wa China kuunga mkono juhudi za Tanzania katika kuimarisha miundombinu ya kisasa ili kujiandaa vyema na uenyeji wa fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2027).

    Wito huo umetolewa hivi karibuni na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, James Millya, wakati wa hafla ya kusherehekea Mwaka Mpya wa China iliyofanyika katika Ubalozi wa nchi hiyo jijini Dar es Salaam.

    Millya amesisitiza kuwa maandalizi ya AFCON 2027 ni zaidi ya michezo, akiyataja mashindano hayo kama fursa ya kimkakati kwa ajili ya mabadiliko ya kiuchumi kwa kuchochea ukuaji wa uchumi kupitia biashara na utalii, upanuzi wa miundombinu ukihusisha ujenzi na ukarabati wa viwanja vinavyokidhi viwango vya kimataifa na kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania, nchi jirani za Afrika Mashariki na washirika wa kimataifa kama China.

    Naibu Waziri amebainisha kuwa uenyeji wa mashindano hayo unahitaji uwekezaji mkubwa katika mifumo ya usafirishaji, huduma za kijamii, na viwanja vya kisasa. China, ikiwa ni mshirika mkuu wa Tanzania katika ujenzi wa miundombinu mikubwa, inatajwa kuwa na mchango muhimu katika kufanikisha azma hiyo ya nchi za Afrika Mashariki.

    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleRASMI AL NASR YAMCHOMOA KIBU DENIS MSIMBAZI KWA MILIONI 776
    Next Article MO DEWJI AHOJI MAGEUZI SIMBA, GUMZO MTANDAONI

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.