Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » SIMBA WABAKI NJIA PANDA, TAFSIRI TOFAUTI YA KAPOMBE
    KITAIFA

    SIMBA WABAKI NJIA PANDA, TAFSIRI TOFAUTI YA KAPOMBE

    By AdminFebruary 9, 2026No Comments1 Min Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    MAHODHA wa Simba, Shomari Kapombe aibua gumzo baada ya kushindwa kuweka wazi maana halisi ya staili yake mpya ya kushangilia mabao, inayohusisha kutembea kama mzee anayesaidiwa na mkongojo, akisema ni staili atakayoendelea nayo kila anapofunga.

    Kapombe alionekana kwa mara ya kwanza akitumia staili hiyo katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Esperance de Tunis, uliochezwa hivi karibuni, ambapo alishangilia kwa namna iliyowaacha wengi njia panda.

    Katika kushangilia huko, beki huyo wa kulia alionekana akishika mfano mkongojo, ishara iliyozua tafsiri tofauti miongoni mwa mashabiki, huku baadhi wakiamini ni ujumbe maalum aliokusudia kuuwasilisha.

    Akizungumza kuhusu staili hiyo, Kapombe amesema  ameamua kuitumia kama sehemu ya kujipa motisha binafsi, hasa kutokana na maneno ya kubezwa anayopata kutoka kwa baadhi ya watu.

    Nahodha huyo wa Simba aliongeza kuwa kila atakapopata nafasi ya kufunga, ataendelea kushangilia kwa staili hiyo ya kutembea kama mzee, kama njia ya kuwajibu wanaomdharau au kumuita mzee.

    “Hivi sasa nawaacha wanaoelewa maana yake waendelee kuelewa kwa njia yao, lakini hapo baadaye nitaweka wazi sababu hasa zilizonifanya nichague hii staili,” amesema  Kapombe.

    Kwa mujibu wa taarifa zilizopo, staili hiyo ya Kapombe inalenga kuwapa majibu wale wanaomkosoa na kumbeza, huku akionyesha kuwa bado ana nguvu, ari na ‘damu inayochemka’ ndani ya uwanja.

    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleMILIONI 500 KUWAPELEKA YANGA ROBO FAINALI
    Next Article Mbwana Samatta na Simon Msuva Hali Ngumu Huko Walipo, Hawatupii Tena

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.