Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home ยป Mbwana Samatta na Simon Msuva Hali Ngumu Huko Walipo, Hawatupii Tena
    KITAIFA

    Mbwana Samatta na Simon Msuva Hali Ngumu Huko Walipo, Hawatupii Tena

    By AdminFebruary 9, 2026No Comments2 Mins Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    LICHA ya nyota wawili Mbwana Samatta na Simon Msuva kuwa na umuhimu mkubwa kwenye kikosi cha timu ya taifa, Taifa Stars takwimu zinaonyesha msimu huu bado hawajaonyesha viwango vikubwa wakiwa kwenye klabu wanazozitumikia.

    Katika mechi 13 alizocheza msimu huu wa Ligi Kuu Ufaransa, mshambuliaji huyo bado hajafunga bao wala kutoa asisti tofauti na msimu uliopita alipokuwa PAOK ya Ugiriki.

    Akiwa PAOK, Samatta alifunga mabao manne na kutoa asisti moja katika mechi 12, takwimu zilizothibitisha bado ana uwezo wa kumalizia nafasi.

    Hata hivyo, ni kama uhamisho wake wa kwenda Le Havre umeambatana na ugumu wa ligi, kasi ya mechi na majukumu ya kucheza nafasi tofauti za ushambuliaji.

    Samatta hatumiki kama mshambuliaji wa mwisho pekee mara nyingi hushuka chini kusaidia ujenzi wa mashambulizi, kufungua nafasi kwa wachezaji wa pembeni na kupambana na mabeki wenye nguvu.

    Hilo limeathiri idadi ya nafasi anazopata za kufunga, lakini halijafuta mchango wake kiufundi ndani ya timu.

    Ndiyo maana licha ya kutofunga mabao, benchi la ufundi la Le Havre limeendelea kumuamini, ishara kwamba nyota huyo anatoa zaidi ya kufunga.

    Download Gospel Songs: https://hizigospel.com/

    Kwa Simon Msuva naye hali si shwari kwani msimu huu amefunga mabao mawili na kutoa asisti nne katika mechi 12, tofauti na msimu uliopita alipofunga mabao 12 katika mechi 11.

    Takwimu zinaonyesha msimu huu ameshuka hasa katika kufumania nyavu za wapinzani tofauti na msimu uliopita ambao alikuwa na wastani wa kufunga bao moja kwa kila mechi.

    Hata hivyo, kubadilishiwa majukumu kwenye kikosi hicho imekuwa moja ya sababu ya nyota huyo kutoanza na makali akitumika zaidi kama mchezeshaji wa pembeni kuliko mshambuliaji.

    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleSIMBA WABAKI NJIA PANDA, TAFSIRI TOFAUTI YA KAPOMBE
    Next Article SIMBA WATIKISWA, YANGA WAPANGIA ROBO FAINALI

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.