Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home ยป RC MAKALLA AKAGUA UWANJA WA AFCON ARUSHA
    KITAIFA

    RC MAKALLA AKAGUA UWANJA WA AFCON ARUSHA

    By AdminSeptember 6, 2025No Comments2 Mins Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Makalla
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Amos Gabriel Makalla leo Ijumaa Septemba 05, 2025 ametembea na kukagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa uwanja wa mpira wa miguu utakaotumika kwenye mashindano ya Mataifa ya Afrika ya AFCON mwaka 2027 unaojengwa na serikali kwa gharama ya Shilingi Bilioni 340, kwenye Kata ya Olmot Jijini Arusha.

    Ukaguzi huo umefanyika baada ya kikao kazi kilichofanyika kikihusisha wakuu wa idara na mamlaka zinazohusika na miundombinu ya huduma za Maji, nishati, barabara na mawasiliano katika uwanja huo, wakiazimia kuteua Kikosi kazi cha wataalamu wa sekta hizo chini ya mwakilishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, ambao watakuwa uwanjani hapo muda wote kushughulikia uwekaji wa miundombinu hiyo chini ya Mpango mkakati wa dharura.

    “Kama Mkoa wa Arusha tunajivunia utalii, Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya mambo mawili Royal Tour, ametangaza utalii na anatuletea Utalii wa michezo (sport tourism) na uwepo wa uwanja huu utaongeza mzunguko wa pesa utakaochochea ukuaji wa biashara na uchumi wa mtu mmoja mmoja na mkoa kwa ujumla, hivyo tunamuhakikisha Mhe. Rais kwamba tutamuwakilisha vyema, tutasimamia ukamilishaji wa uwanja huu ili kuhakikisha malengo aliyotarajia yanatimia na mkandarasi ametuhakikishia kwamba utakamilika kama ilivyopangwa Julai 2026.” Amesema Mhe. Makalla.

    Aidha Mhe. Makalla amesisitiza kuwa uwanja ni mkubwa na wa kisasa wenye kukidhi viwango vya Shirikisho la soka barani Afrika CAF, akisema maamuzi haya ya Rais Samia ya kutumia mapato ya serikali kuujenga uwanja huo yanakwenda kuipa heshima Tanzania na kuwapa fursa wananchi wa Arusha na watanzania kwa ujumla kuweza kushuhudia mashindano hayo nchini mwao, yakifanyika kwa ushirikiano wa Mataifa ya Tanzania, Kenya na Uganda.

    Hata hivyo Mwakilishi wa mkandarasi anayetekeleza mradi huo China Railway Construction ya nchini China Mhandisi Denice Benito Mtemi amesema ujenzi wa mradi huo umefikia asilimia 60 ukitarajiwa kujumuisha nyasi asili kwenye sehemu ya kuchezea.

    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleCLATOUS CHAMA KUWAPA FURANGA SINGIDA BLACK STARS
    Next Article MIKE TYSON KUZICHAPA NA FLOYD MAYWEATHER

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.