Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » RASMI: YANGA YAMNASA CASEMIRO WA ZANZIBAR KUTOKA MLANDEGE!
    KITAIFA

    RASMI: YANGA YAMNASA CASEMIRO WA ZANZIBAR KUTOKA MLANDEGE!

    By AdminJuly 24, 20251 Comment1 Min Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    yanga
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    Klabu ya Yanga imeendelea kujiimarisha kuelekea msimu mpya baada ya kumtambulisha rasmi kiungo mkabaji wa Mlandege, Abdulnassir Mohammed Abdallah, maarufu kama “Casemiro”, kwa mkataba wa miaka mitatu.

    Usajili wa kiungo huyo mahiri ulimalizika tangu Julai 2, 2025, lakini klabu hiyo imemtambulisha rasmi leo, ikiwa ni sehemu ya mipango yao ya kusuka kikosi imara na chenye ushindani wa hali ya juu.

    Katika kumsajili, Yanga walishinda vita kali ya saini yake dhidi ya klabu kama Azam FC, JKT Tanzania na Singida Black Stars, ambazo zote zilikuwa kwenye harakati za kumchukua kiungo huyo tegemeo kutoka Zanzibar.

    Abdulnassir, anayefahamika kwa jina la utani la “Casemiro” kutokana na aina yake ya uchezaji wa kukaba kwa ufanisi, ni kipaji kipya kilichotoka visiwani Zanzibar, na anaonekana kuwa na uwezo mkubwa wa kuziba nafasi ya kiungo mkabaji ndani ya kikosi cha Wananchi.

    Usajili huu unaashiria dhamira ya Yanga ya kuendelea kuwa na safu thabiti ya kiungo, huku wakijihakikishia nguvu mpya itakayowasaidia katika mashindano ya ndani na ya kimataifa.

    Yanga SC
    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleYANGA SC YAMALIZANA NA MASHINE YA MABAO
    Next Article MAGAZETI YA MICHEZO LEO ALHAMISI TAREHE 24-7-2025

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    View 1 Comment

    1 Comment

    1. Pingback: MAGAZETI YA MICHEZO LEO ALHAMISI TAREHE 24-7-2025 - SOKALEO

    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.