Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » MWENDO WA KIMYA KIMYA AISEE…SIMBA WASHUSHA MASHINE HII MPYA YA KAZI DAR….
    KITAIFA

    MWENDO WA KIMYA KIMYA AISEE…SIMBA WASHUSHA MASHINE HII MPYA YA KAZI DAR….

    By AdminOctober 15, 2025No Comments2 Mins Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    simba
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    MABORESHO ya benchi la ufundi la Simba yanaendelea, baada ya ujio wa Dimitir Pantev na msaidizi wake, Simeonov Boyko Kamenov waliotokea Gaborone United ya Botswana, sasa ameshushwa mtu mwingine.

    Simba SC imemshusha kwa siri sana kocha wa makipa kutoka Bulgaria kwa ajili ya kuimarisha benchi la ufundi la timu hiyo linaloongozwa na Dimitir Pantev.

    Mtaalamu huyo aliyetua majira ya saa 9:05 alfajiri na ndege ya Shirika la Uturuki, ni Vitomir Vutov mwenye umri wa miaka 53 ambapo amekuja kuungana na wenzake siku chache baada ya kuondoka kwa Fadlu Davids.

    Ujio wa Vutov, unalifanya benchi la ufundi la Simba kuwa na raia watatu kutoka Bulgaria, wengine ni Pantev aliyetambulishwa kama Meneja Mkuu na msaidizi wake, Simeonov Boyko Kamenov.

    “Ni kweli jamaa amekuja na leo (juzi) asubuhi amefika uwanja wa mazoezi kutambulishwa kwa wachezaji,” kimesema chanzo kutoka Simba.

    “Amekuja kwa ajili ya kuwafundisha makipa kwa sababu nafasi hiyo haikuwa na kocha baada ya Fadlu kuondoka na wasaidizi wake.”

    Hata hivyo, Simba inafanya siri sana juu ya ujio wa kocha huyo huku ikielezwa muda wowote atatambulishwa.

    Vutov ambaye rekodi zinaonyesha mara ya mwisho alikuwa na kikosi cha FC Lovech huko Bulgaria, anakuja kuchukua nafasi ya Wayne Sandilands ambaye ameondoka na Fadlu kuelekea Raja Casablanca.

    Rekodi zinaonyesha Vutov kabla ya kutua Simba, amepita kufundisha klabu kadhaa ikiwemo Spartak Varna, PFC Lokomotiv Plovdiv, FC Lokomotiv Gorna Oryahovitsa, Litex Lovech zote za Bulgaria.

    Septemba 22, 2025, wakati Fadlu anaaga ndani ya Simba, aliondoka na wasaidizi wake wanne ambao ni Darian Wilken (Kocha Msaidizi), Wayn Sandilands (Kocha wa Makipa), Durell Butler (Kocha wa Utimamu) na Mueez Kajee (Mchambuzi wa Video).

    Kuondoka kwa Fadlu na wasaidizi wake, imeifanya Simba kuboresha benchi la ufundi ambapo sasa Seleman Matola aliyeendelea kubaki kama kocha msaidizi, Pantev amekuja na msaidizi wake mwingine aliyekuwa naye Gaborone United. Pia Vutov ametua kwa ajili ya kuwanoa makipa, huku kocha wa utimamu akipewa jukumu hilo amepewa mzawa, Mohamed Mrishona Mohamed ‘Xavi’.

    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleUWANJA WA SOKOINE WAFUNGIWA KUCHEZWA MECHI ZA LIGI KUU
    Next Article SIMBA JOTO LAPAMBA MOTO KUELEKEA MECHI DHIDI YA NSINGIZINI

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.