Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home ยป MOHAMED HUSSEIN AFICHUA VITA YAKE NA BOKA INAYOENDELEA YANGA
    KITAIFA

    MOHAMED HUSSEIN AFICHUA VITA YAKE NA BOKA INAYOENDELEA YANGA

    By AdminSeptember 24, 2025No Comments2 Mins Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    MOHAMED HUSSEIN
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    Beki mpya wa Yanga, Mohamed Hussein ‘Tshabalala’, amefunguka kuwa ni kweli kuna ushindani mkali wa namba kati yake na Chadrack Boka, lakini pia akieleza hadhani kama atakuwa anaanzia benchi mechi zote kwani kuna mashindano mengi sana mbele yao.

    Tshabalala, aliyejiunga na Yanga msimu huu akitokea Simba, amebainisha kuwa kwenye kikosi chote cha Yanga kuna ushindano mkali wa namba kwenye idara zote na si eneo analocheza yeye, hivyo Kocha Mkuu, Romain Folz, ndiye atakayekuwa akiamua nani anaanza na nani aingie baadaye.

    Beki huyo wa kushoto, alisema hayo kutokana na kuonekana akianzia benchi kwenye mechi tatu ambazo Yanga imecheza mpaka sasa.
    “Mwalimu ndiye atakuwa anachagua nani aanze nani amalize, timu hii imekamilika kila idara, ina wachezaji bora zaidi ya mmoja na yeyote anayeanza timu inapata ushindi.

    “Kwa maana hiyo ni kwamba kweli kuna ushindani wa namba, lakini si kila siku atakayeanza basi atakuwa anaanza mechi zote, mashindano yako mengi sana, naamini kila mtu atapata nafasi ya kuanza na kucheza mechi nyingi kadri iwezekanavyo,” alisema beki huyo wa kushoto ambaye pia huichezea Timu ya Taifa Stars.

    Katika mechi ya kilele cha Wiki ya Mwananchi dhidi ya Bandari ya Kenya, Ngao ya Jamii dhidi ya Simba na mchezo wa kwanza hatua za awali, Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Wiliete de Benguela ya Angola, mchezaji huyo ambaye pia hutumia jina la Zimbwe Jr, zote hizo aliingia kipindi cha pili kama mchezaji wa akiba, hivyo kuzua minong’ono kwa baadhi ya mashabiki kuwa amekuwa mchezaji wa akiba, badala ya kuanza michezo yote kama alivyokuwa Simba.

    Yanga SC
    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleEDO KUMWEMBE: SIJAONA CHOCHOTE KWA KOCHA FADLU
    Next Article SERIKALI YATOA KAULI JUU YA SAKATA LA PAMBA JIJI KUFANYA MAZOEZI GIZANI

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.