Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » EDO KUMWEMBE: SIJAONA CHOCHOTE KWA KOCHA FADLU
    KITAIFA

    EDO KUMWEMBE: SIJAONA CHOCHOTE KWA KOCHA FADLU

    By AdminSeptember 24, 2025No Comments2 Mins Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Fadlu
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    Sidhani kama Simba wana kitu kikubwa cha kupoteza katika hili. Kuna kocha huwa anawaweka katika wakati mgumu akiamua kuondoka zake. Kuna aina ya mpira anaweza kuondoka nayo. Hadi sasa hatutajua mpira wa Fadlu ni upi hasa. Kuanzia pale alipoishika timu na mpaka pale alipokwenda likizo kisha akarudi, akahusika katika usajili na kisha kwenda na timu kambini Misri.

    Wakati ikiwa pale Ismailia chini ya Fadlu sidhani kama Simba imetengeneza aina yoyote ya mpira wa kushtua chini ya Fadlu. Siku hizi makocha wanatengeneza falsafa zao. Unaweza kuchagua kuwa bora katika kushambulia, au kukaa na mpira, au kujihami. Sijaona LOLOTE ambalo Fadlu amelitengeneza kwa ufasaha wakati timu ikiwa kambini kule Misri.

    Tukianzia mechi ya Gor Mahia katika siku ya Simba Day. Wageni waliwafundisha wenyeji namna ya kukaa na mpira kwa muda mrefu. Bahati mbaya tu wageni waliruhusu mabao mawili. Halafu likaja pambano la Simba na Yanga. Simba walionekana kucheza vizuri. Sio kwamba walikuwa wazuri, hapana, ni vile tu Yanga walitarajiwa kuwa wazuri zaidi ya Simba lakini hawakucheza katika kiwango chao. Bado mwisho wa yote Fadlu aliendelea kuweka rekodi ya kupoteza pambano jingine la Dabi dhidi ya mtani kitu ambacho kimekuwa cha kawaida kwake.

    Na Jumamosi jioni Simba ilikuwa Gaborone ikicheza pambano la kimataifa la ushindani dhidi ya Gaborone United Simba haikuonyesha kama ilikuwa kambini Misri ikipika kitu. Ilicheza ovyo ingawa ilishinda 1-0. Sijakutana na shabiki wa Simba aliyeridhika na kiwango cha timu

    Kama akiondoka sasa Simba watakuwa katika nafasi nzuri ya kuanza na kocha mpya kabla msimu haujachanganya. Labda wachezaji watamuelewa mapema kocha mpya wakati msimu angali ukiwa mchanga.”

    — Legend, Edo Kumwembe. [JichoLaMwewe]

    Simba SC
    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleHAYA HAPA MAGAZETI YA LEO SEPTEMBA 24, 2025
    Next Article MOHAMED HUSSEIN AFICHUA VITA YAKE NA BOKA INAYOENDELEA YANGA

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.