Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » MAVAMBO AMALIZA SAFARI YAKE SIMBA SC, ATOA UJUMBE WA KUAGA
    KITAIFA

    MAVAMBO AMALIZA SAFARI YAKE SIMBA SC, ATOA UJUMBE WA KUAGA

    By AdminJuly 19, 2025No Comments2 Mins Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    Kiungo fundi wa kimataifa, Debora Fernandes Mavambo (24), mwenye uraia pacha wa Congo-Brazzaville na Gabon, ameaga rasmi klabu ya Simba SC, takribani mwaka mmoja tu tangu asajiliwe kwa mkataba wa miaka mitatu akitokea Mutondo Stars ya Zambia.

    Mavambo ambaye anachezea timu ya taifa ya Gabon, ametangaza kuondoka kwake kupitia ujumbe wa kuushukuru uongozi na mashabiki wa klabu hiyo maarufu ya Msimbazi, akisisitiza kuwa ataikumbuka Simba daima kwa sapoti na mapokezi aliyoyapata wakati wote wa uwepo wake.

    “Asante sana familia ya Simba SC kwa sapoti yao katika kipindi chote nilichokuwa ndani ya klabu hii. Hakika nitaikumbuka klabu hii, mashabiki na viongozi wote wa Simba Sport Club,” alisema Mavambo kupitia ukurasa wake wa mitandao ya kijamii.

    Nyota huyo mwenye kipaji kikubwa katika eneo la kiungo cha kati, alisajiliwa na Simba kwa matarajio makubwa ya kuimarisha safu ya kiungo lakini safari yake imekatika kabla ya kukamilika kwa mkataba wake wa awali.

    Hadi sasa haijafahamika rasmi sababu za kuondoka kwake mapema, lakini taarifa za ndani ya klabu zinaashiria uwezekano wa pande hizo mbili kufikia makubaliano ya kuvunja mkataba kwa makubaliano maalum.

    Kuondoka kwa Mavambo kunafungua nafasi katika kikosi cha Simba kinachoendelea na mchakato wa usajili na maandalizi ya msimu mpya wa 2025/26, ambapo klabu hiyo imekuwa ikifanya mabadiliko kadhaa ndani ya kikosi chake kuelekea kampeni mpya za ndani na kimataifa.

    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleVIPERS SC YAMSAJILI WINGA MNIGERIA ODILI CHUKWUMA KWA MKATABA WA MIAKA MIWILI
    Next Article SIMBA WA AHAHIDI KUFANYA KWELI KWENYE USAJILI

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.