Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » FOLZ ANAJIPANGA KUENDELEZA REKODI YA KUISULUBU SIMBA – KAMWE
    KITAIFA

    FOLZ ANAJIPANGA KUENDELEZA REKODI YA KUISULUBU SIMBA – KAMWE

    By AdminSeptember 3, 2025No Comments2 Mins Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    Klabu ya Yanga imesema haifanyi utani kuelekea mchezo wa Ngao ya Jamii, hivyo Kocha Mkuu, Romain Folz, amekuwa na ‘programu’ nne tofauti za maandalizi kuelekea mechi hiyo inayotarajiwa kupigwa, Septemba 16, mwaka huu, katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

    Ofisa Habari wa Klabu hiyo, Ali Kamwe, amesema kocha wa timu hiyo amekuwa na mazoezi ya gym, ufukweni, uwanjani na darasani kwa ajili ya mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Simba ambao utakuwa unaashiria kuanza kwa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu mpya, Septemba 17, mwaka huu.

    Kamwe amesema kocha Romain anataka kuendeleza rekodi za makocha wenzake, Miguel Gamondi na Miloud Hamdi, ambao walikuwa wakiisulubu Simba kila wanapokutana.

    Alisema anataka kuendeleza rekodi ya Yanga kuifunga Simba, ambapo kama atafanikiwa itakuwa ni mara ya sita mfululizo kwa timu yao kuwafunga watani wao wa jadi.

    “Timu inaendelea vizuri kumekuwa na programu tofauti tofauti za uwanjani, gym, ufukweni na darasani, huu ni mwendelezo wa maandalizi hasa kuelekea kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Simba, ingawa tuna mchezo dhidi ya Bandari ya Kenya kwenye kilele cha Wiki ya Mwananchi.

    “Mwalimu ni mpya na wasaidizi wake ni wapya, hilo linakupa picha kwamba wanataka kufanya vizuri. Mwalimu nimemwangalia ana vitu vingi, ana mbinu nyingi sana ambazo zitaanza kuonekana Wiki ya Mwananchi, Ngao ya Jamii na hata kwenye michezo ya kimataifa,” alisema Kamwe.

    Yanga SC
    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleRAMOS ALIUMIA SANA KUONDONA MADRID
    Next Article AUDIO Paul Clement – In You MP3 DOWNLOAD

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.