Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » FEISAL SALUM AFICHUA HESABU ZA TANZANIA CHAN 2024
    KITAIFA

    FEISAL SALUM AFICHUA HESABU ZA TANZANIA CHAN 2024

    By AdminAugust 20, 2025No Comments1 Min Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    WAKATI Tanzania Agosti 16 2025 kwenye mchezo wa CHAN 2024 ikishuhudia ubao wa Uwanja wa Mkapa ukisoma Afrika ya Kati 0-0 Tanzania, kiungo Feisal Salum amebainisha kuwa watapambana katika hatua ya robo fainali kupata matokeo mazuri.

    Mchezo huo uliopita hatua ya makundi ulikuwa wa kwanza kwa Tanzania kugawaa pointi mojamoja. Katika mechi tatu ambazo zilipita za makundi Tanzania ilishinda zote ikikusanya pointi 9.

    Baada ya mechi nne, Tanzania inaongoza kundi B ikiwa na pointi 10 itacheza na Morocco hatua ya robo fainali mchezo unaotarajiwa kuchezwa Agosti 22, 2025 Uwanja wa Mkapa.

    Nyota huyo ambaye alichaguliwa kuwa mchezaji bora baada ya mchezo alibainisha kuwa wanatambua kuna kazi kubwa mbele yao hivyo watapambana kuwa bora zaidi.

    “Kwenye mchezo wetu uliopita haikuwa shida katika kutafuta matokeo kwa kuwa tulienda na game plan yetu ya kile ambacho tulifundishwa mazoezini. Ambacho walifanya wapinzani wetu ni kuziba nafasi ambazo tulizifanyia mazoezi. Mimi mchezaji katika matokeo tuliyopata hatujaridhika.

    “Tulitegemea matokeo kwenye mchezo wetu. Wenzetu walituheshimu na kuja kwa umakini. Mchezo huu umepita tunaangalia mechi zijazo hatua ya robo fainali. Tunaamini tutapambana kufanya vizuri zaidi, “ amesema Fei Toto

    Kocha Mkuu wa Tanzania, Hemed Suleman ameweka wazi kuwa makosa yaliyopita watafanyia kazi ili kupata matokeo kwenye mechi zijazo.

    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleSIMBA SC KUZINDUA UZI MPYA AGOSTI 27 2025
    Next Article ISAK AVUNJA UKIMNYA, ADAI KUNA USALITI UMEFANYIKA

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.