Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home ยป Cv ya Dimitar Pantev Kocha Mpya wa Simba Sc 2025
    KITAIFA

    Cv ya Dimitar Pantev Kocha Mpya wa Simba Sc 2025

    By AdminOctober 3, 2025No Comments2 Mins Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    Cv ya Dimitar Pantev Kocha Mpya wa Simba Sc 2025

    Klabu ya Simba SC imethibitisha rasmi kumteua Dimitar Pantev kuwa kocha mkuu mpya wa timu hiyo kwa msimu wa 2025, akichukua mikoba iliyoachwa wazi na Fadlu Davids aliyetimkia Raja Casablanca ya Morocco.

    Pantev, raia wa Bulgaria mwenye umri wa miaka 49, anakuja nchini akiwa na rekodi ya mafanikio barani Afrika baada ya kuinoa klabu kadhaa na kushinda mataji ya ligi katika mataifa mawili tofauti.

    Kocha huyu aliyetambulika kwa falsafa yake ya soka la kushambulia, amesaini mkataba wa miaka miwili na Simba SC, klabu inayolenga kurejea kwenye utawala wa soka la Tanzania na pia kufanya vizuri katika michuano ya kimataifa ya CAF.

    Wasifu wa Dimitar Pantev

    • Jina kamili: Dimitar Pantev
    • Umri: Miaka 49
    • Tarehe ya kuzaliwa: 26 Juni 1976
    • Mahali: Varna, Bulgaria
    • Uraia: Bulgaria
    • Leseni: Leseni ya UEFA Pro (ngazi ya juu ya ukocha barani Ulaya)

    Safari ya Dimitar Pantev Kama Kocha

    Dimitar alianza kazi yake ya ukocha katika kikosi cha vijana cha Varna City. Baada ya hapo, alijiunga na klabu ya Al Ahli Hebron kama Kocha Msaidizi kabla ya kupata nafasi ya kuongoza vikosi vya wakubwa kama Flamengo, Victoria United, Johansen, Orapa, na hatimaye Gaborone United.

    Dimitar Pantev ameonyesha ujuzi mkubwa katika kazi yake ya ukocha hususan barani Afrika. Kabla ya kutua Simba SC, ameifundisha jumla ya klabu tano barani humo. Safari yake imeanzia Victoria United (Cameroon) ambako alikiongoza kikosi hicho kubeba ubingwa wa kwanza katika historia ya klabu hiyo. Baada ya hapo alihamia FC Johansen (Sierra Leone), kisha Orapa United na Gaborone United zote za Botswana.

    Akiwa na Gaborone United, alifanikiwa kuipa klabu hiyo ubingwa wa 8 wa Ligi Kuu ya Botswana, jambo lililomfanya kujiimarisha zaidi kama kocha mwenye rekodi ya mafanikio. Kwa kipindi cha miaka mitano barani Afrika, amebeba mataji mawili ya Ligi Kuu katika mataifa mawili tofauti, ikiwemo Cameroon na Botswana.

    Mbali na soka la kawaida, Pantev pia ana historia kubwa katika mchezo wa Futsal. Akiwa kocha, ameiongoza timu yake kutwaa mataji matano ya Ligi Kuu ya Bulgaria ya Futsal, jambo linaloonyesha upeo wake mpana wa kiufundi katika michezo tofauti.

    Historia ya Dimitar Pantev Akiwa Kama Mchezaji

    Kabla ya kuwa kocha, Dimitar Pantev aliwahi kucheza soka kwenye nafasi ya kiungo. Alicheza katika ngazi ya Ligi Kuu nchini Bulgaria, akipita katika timu kadhaa ikiwemo:

    • Cherno More
    • FC Suvolovo
    • Chernomorets Byala
    • Kaliakra Kavarna
    • Chernomorets Balchik
    • Volov Shumen
    • Dobrudzha
    • Vladislav
    • Shabla
    • Spartak Varba
    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleHAYA HAPA MAGAZETI YA LEO OKTOBA 3, 2025
    Next Article MAKOCHA WA MAPACHA WA KARIAKOO KUPISHANA AIRPORT

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.