Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » BARKER AWEKA WAZI SIRI YA HOFU, KABLA YA DERBY
    KITAIFA

    BARKER AWEKA WAZI SIRI YA HOFU, KABLA YA DERBY

    By AdminFebruary 23, 2026No Comments2 Mins Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    KOCHA Mkuu wa Simba SC, Steve Barker, ameweka wazi kuwa ubora wa viwanja vinavyotumika katika mechi za Ligi Kuu Bara ndiyo jambo linalompa wasiwasi mkubwa kwa sasa, hasa katika kipindi hiki ambacho timu yake inaelekea kwenye michezo muhimu.

    Barker amesema hali ya baadhi ya viwanja inampa hofu kuhusu usalama wa wachezaji wake, kuwa jambo la msingi kwake ni kuhakikisha kikosi chake kinamaliza mechi kikiwa salama bila majeraha, hususan kuelekea michezo mikubwa ikiwemo Kariakoo Derby.

    Ameeleza kuwa viwanja vyenye mashimo au nyasi zisizo katika hali nzuri vinaweza kusababisha madhara makubwa kwa wachezaji, hasa wanapokutana na timu zinazocheza soka la nguvu.

    “Nazingira hayo humuweka mchezaji katika hatari ya kuumia kirahisi, Ukiniuliza kitu gani kinachonipa presha kwa sasa ni ubora wa viwanja.

    Sitamani mchezaji wangu yeyote apate jeraha. Kiwanja chenye mashimo au nyasi mbovu kinaweza kusababisha maumivu na kuathiri mipango yetu,” amesema Barker.

    Hata hivyo, pamoja na changamoto hizo, kocha huyo ameonyesha imani kubwa kwa kikosi chake amesisitiza kuwa lengo la Simba ni kuhakikisha wanapambana na kubeba alama tatu katika kila mchezo.

    Amesema wachezaji watakaopangwa lazima wawe fiti, wafuate maelekezo ya benchi la ufundi na kucheza kwa nidhamu na umakini mkubwa.

    Barker ameongeza kuwa ushindani wa ligi ni mkubwa na mechi zijazo zitakuwa ngumu, lakini anaamini wachezaji wake wanafahamu thamani ya jezi wanayoivaa na wajibu wao kwa mashabiki na klabu kwa ujumla.

    Kwa mtazamo wake, licha ya presha ya ushindani na changamoto za miundombinu, Simba itaendelea kupambana kufikia malengo yake, huku akitanguliza usalama wa wachezaji kama kipaumbele cha kwanza.

    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleMgombea Urais Barcelona Victor Font Aahidi Kumrejesha Messi Camp Nou
    Next Article SIMBA YALENGA DODOMA, DERBY SIO KIPAUMBELE

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.