Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » Aziz Ki aandika ujumbe mzito kwa Hamisa Mobetto siku yake ya kuzaliwa.
    KITAIFA

    Aziz Ki aandika ujumbe mzito kwa Hamisa Mobetto siku yake ya kuzaliwa.

    By AdminDecember 11, 2025No Comments2 Mins Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    Mchezaji wa zamani wa Yanga anayekipiga klabu ya Wydad kwa sasa Stephane Aziz Ki ameandika ujumbe mzito kwenye ukurasa wake wa Instagram akimtakia kila la kheri mke wake mwanamitindo wa Tanzania Hamisa Mobetto katika kumbukumbu ya siku yake ya kuzaliwa.

    Aziz Ki ambaye alifunga ndoa na mwanamitindo huyo wa Tanzania mapema mwaka huu kwa sasa anakipiga Nchini Morocco huku mpaka sasa wakiwa bado hawajajaliwa kupata mtoto pamoj licha ya kila mmoja kuwa na watoto nje ya ndoa yao.

    “Mpenzi wangu Hamisamobetto,
    Katika siku hii maalum, nataka nikukumbushe umuhimu wako maishani mwangu. Kila mwaka nikiwa pembeni yako ni zawadi ya thamani—sura mpya iliyojaa mapenzi, furaha, na kumbukumbu zisizosahaulika.

    Wewe ni nguvu yangu, upole wangu, amani yangu, na msukumo wangu. Kwa sababu yako mimi ni mwanaume bora, na kila muda ninaokuona hunikumbusha jinsi nilivyo barikiwa kukupenda na kupendwa na wewe.

    Leo, siadhimishii tu siku yako ya kuzaliwa… ninaadhimisha mwanamke wa kipekee uliye: moyo wako mkarimu, tabasamu lako la faraja, ujasiri wako, nuru yako, na namna uwepo wako unavyoangaza maisha yangu.

    Naomba mwaka huu mpya wa maisha yako uje na furaha zaidi, mafanikio, amani, na upendo. Na ujue kwamba daima nitakuwa hapa kando yako—kukupenda, kukusaidia, na kukuthamini jinsi unavyostahili.

    Heri ya Siku ya Kuzaliwa, malkia wangu.

    Nakupenda zaidi ya maneno yanavyoweza kuelezea,
    MIRS KI”Ameandika Azizi Ki.

    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleDavies arejea uwanjani baada ya kuuguza goti kwa siku 262
    Next Article Chico Ushindi Afariki, Soka la Afrika Lapata Pengo

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.