Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » Arsenal Warejea Kileleni EPL Baada ya Ushindi Mwembamba Dhidi ya Everton
    KIMATAIFA

    Arsenal Warejea Kileleni EPL Baada ya Ushindi Mwembamba Dhidi ya Everton

    By AdminDecember 21, 2025No Comments1 Min Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Arsenal
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    Arsenal wamerejea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya England (EPL) kufuatia ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya Everton katika dimba la Hill Dickinson, jijini Liverpool.

    Bao pekee la mchezo lilifungwa dakika ya 27 na Viktor Gyökeres kwa mkwaju wa penalti, bao lililotosha kuwapa The Gunners alama zote tatu muhimu.

    Kwa ushindi huo, Arsenal wamefikisha pointi 39 baada ya michezo 17, wakipanda hadi nafasi ya kwanza, alama mbili mbele ya Manchester City, ambao wameshuka hadi nafasi ya pili baada ya kukaa kileleni kwa muda mfupi.

    Everton walijitahidi kusaka bao la kusawazisha hasa kipindi cha pili, lakini safu ya ulinzi ya Arsenal iliendelea kuwa imara na kuhakikisha wageni wanaondoka na ushindi.

    Matokeo hayo yanaendeleza ushindani mkali kileleni mwa EPL huku mbio za ubingwa zikizidi kuchangamka.

    FT: Everton 0-1 Arsenal
    ⚽ 27’ Gyökeres (P)

    Arsenal FC
    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleHii Hapa Ratiba ya AFCON 2025
    Next Article Jumapili ya Soka Ulaya: Mechi Kubwa Bundesliga, Serie A na LaLiga

    Related Posts

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    March 18, 2026

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    March 18, 2026

    Drone Yashambulia Tangi la Mafuta Karibu na Uwanja wa Ndege wa Dubai.

    March 16, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.