Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » YANGA YAPATA USHINDI WAKE WA KWANZA KIMATAIFA
    KITAIFA

    YANGA YAPATA USHINDI WAKE WA KWANZA KIMATAIFA

    By AdminSeptember 19, 2025No Comments4 Mins Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    FT: Wiliete SC 0-3 Yanga SC

    Dakika ya 88 nahodha wa Wiliete anaonyeshwa kadi ya njano kwa kumchezea faulo nyota wa Yanga SC

    Dakika ya 86 Yanga SC wanapata pigo huru nje kidogo ya 18 linapigwa na Ecua.

    Goooooal Yanga SC

    Dakika ya 82 Prince Dube anafunga goal la 3 kwa Yanga SC akiwa ndani ya 18

    Dakika ya 75 mfungaji wa bao la kwanza kwa Yanga SC, Aziz anatoka nafasi yake inachukuliwa na Conte, Zimbwe Jr naye anaingia akichukua nafasi ya Boka., Duke Abuya anakuwa mchezaji wa kwanza kuonyeshwa kadi ya njano kwenye mchezo wa leo.

    Goooooal Yanga SC

    Dakika ya 72 Edmund John anafunga goal la pili kwa Yanga SC akitumia pasi ya Maxi Nzengeli

    Dakika ya 70 Pacome anakwenda nje nafasi yake inachukuliwa na Celestin Ecua

    Dakika ya 69 Yanga SC wanapata kona inapigwa na Pacome

    Dakika ya 66 Edmund John anapewa jukumu la kupiga kona iliyosababishwa na beki wa Wiliete baada ya kuokoa krosi iliyopigwa na Boka.

    Dakika ya 62 Edmund anafanya jaribio akiwa ndani ya 18 linaokolewa na mlinda mlango wa Wiliete, nyota wawili wa Wiliete ikiwa ni Daniel Nicholas  wanapata maumivu kwenye harakati za kuokoa.

    Dakika ya 61 Israel Mwenda anapiga krosi inakutana na Edmund John jaribio lake linaokolewa na mlinda mlango wa Wiliete.

    Dakika ya 59, Maxi anaingia anatoka Mzize

    Edmund John anaingia anatoka Doumbia

    Dakika ya 58 Thobias anapeleka mashambulizi kwa Yanga SC, kiungo mshambuliaji wa Wiliete alifanya jaribio halikuwa na faida.

    Dakika ya 55 Djigui Diarra anapeleka mashambulizi mbele na mpira unamfikia Mzize

    Dakika ya 50 Wiliete SC wanafanya jaribio ambalo linakwenda nje kidogo ya 18

    Dakika ya 48 Thobias anapeleka mashambulizi Yanga SC, Junior anaokoa krosi ya Mwenda na Yanga SC wanapata kona inapigwa na Doumbia inaokolewa na mlinda mlango.

    Dakika ya 47 Aziz Andambwile anaanzisha mashambulizi, Doumbia anampa pasi Dube akiwa ndani ya 18 jaribio lake linaokolewa na mlinda mlango wa Wiliete SC.

    Kipindi cha pili

    Eddy anakwenda benchi kwa Wiliete na dakika 45 zinakwenda kuanza kutoka Angola

    Mapumziko

    Dakika 45 zimekamilika, Wiliete SC 0-1 Yanga SC, goal kwa Yanga SC limefungwa na Aziz Andambwile akiwa nje ya 18.

    Dakika ya 45 Bacca anaokoa hatari, Mzize anapata maumivu

    Dakika ya 44 Agustino anaokoa hatari na kuanzisha mashambulizi haraka kuelekea lango la Yanga SC

    Dakika ya 42 Pacome anatoa krosi kwa Dube akiwa ndani ya 18 jaribio lake linaokolewa na mlinda mlango wa Wiliete.

    Dakika ya 40 Yanga SC wanapata kona, kipa wa Wiliete ameokoa hatari nne ambazo zilikuwa zinakwenda kwenye lango

    Dakika ya 39 nahodha wa Wiliete anatoa mpira nje inakuwa kona kwa Yanga SC, Dube anafanya jaribio kwa pigo la kichwa akitumia krosi ya Pacome inaokolewa na mlinda mlango.

    Dakika ya 38 Thobias wa Wiliete anaokoa krosi iliyopigwa na Israel Mwenda

    Dakika ya 37, Pacome anatoa pasi kwa Dube pembeni inaokolewa

    Dakika ya 36 Wiliete wanafanya jaribio kuelekea lango la Yanga SC

    Goooal Yanga

    Dakika ya 31 Aziz Andambwile anafunga goal kwa Yanga SC akiwa nje ya 18 likimshinda mlinda mlango wa Wiliete SC.

    Dakika ya 30 Pacome anatengeneza pasi nzuri ndani ya 18 kwa Wileiete inaokolewa na Jr

    Dakika ya 28 pasi ya maelekezo kutoka kwa Doumbia inamkuta Mzize ndani ya 18, anafanya jaribio kwa mguu wake wa kushoto linakwenda nje ya 18

    Dakika ya 26 Pacome anapiga krosi kuelekea ndani ya eneo la 18 kwa Wiliete SC inaokolewa

    Dakika ya 25 Duke Abuya anachezewa faulo, kipa wa Wiliete SC anawapanga wachezaji wake na nyuma ya mpira yupo Pacome na Doumbia

    Dakika ya 21 Prince Dube anafanya jaribio kuelekea Wiliete linaokolewa na kipa wa Wiliete SC

    Dakika ya 20 Pacome anafanya jaribio ndani ya 18 linaokolewa na kipa wa Wiliete SC

    Dakika ya 19 Yanga SC inapata kona inapigwa na Doumbia, Wiliete SC wanaokoa

    Dakika ya 16 Duke Abuya anacheza faulo kwa mchezaji wa Wiliete SC

    Dakika ya 13 Yanga SC wanatengeneza nafasi nzuri yakufunga Clement Mzize akiwa ndani ya 18 anakwama kufanya jaribio linakwenda nje ya 18

    Dakika ya 12 Aziz Andambwile anampa pasi Nondo ambaye anapeleka mpira mbele , Abuya anacheza faulo kwa nyota wa Wiliete

    Dakika ya 11 Agustino kipa wa Wiliete anapeleka mashambulizi mbele

    Dakika ya 9 Wiliete wanapata kona ya kwanza iliyosababishwa na Boka, Diarra anaokoa pigo hilo

    Dakika ya 7 Bakari Nondo anapeleka mashambulizi mbele ya Wiliete, Clement Mzize anafanya jaribio kwa pigo la kichwa linakwenda nje ya lango

    Dakika ya 5 Prince Dube anafanya jaribio ambalo halileti matunda

    Dakika ya 4 Clement Mzize anachezewa faulo nje kidogo ya 18

    Dakika ya nne Wiliete wanarudisha mpira kwa kipa Agustino Kalougha

    Dakika ya tatu Yanga SC wanapiga faulo ya kwanza kupitia kwa Doumbia

    Wiliete SC 0-0 Yanga SC, mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika

    Ni katika Estadio 11 de Novembro nchini Angola wakicheza na Wiliete Sports Clube.

    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleORODHA YA WACHEZAJI WA SIMBA SC WALIOPO BOTSWANA
    Next Article SIMBA IPO KAMILI KUWAVAA GABORONE LEO, MECHI YA KIMATAIFA

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.