Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » YANGA WANAMTAFUTA MWENYE KISU KIKALI KUMCHUKUA MZIZE
    KITAIFA

    YANGA WANAMTAFUTA MWENYE KISU KIKALI KUMCHUKUA MZIZE

    By AdminAugust 11, 2025No Comments1 Min Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Yanga
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    ….. OFA IMEKATALIWA. Jana tulilala na neno hili.

    Barua za Waarabu zimeendelea kupishana pale Jangwani. Inaingia barua hii, baada ya muda inaingia barua nyingine. Zote zinazungumzia upatikanaji wa Mzize.

    Wanachokifanya Yanga SC ni kumtafuta yule mwenye kisu kikali ndio ale nyama. Mimi siamini kama Mzize atacheza Yanga SC msimu ujao. Hili siamini, lakini wanachokifanya Yanga SC ni kuiongezea thamani biashara ya Mzize. Itafika tu timu ambayo itatoa ofa ya maana na itakuwa ngumu ofa hiyo kukataliwa. Uzuri Mzize mwenyewe anazidi kuichonganisha biashara yenyewe. Juzi ametupia mabao mawili katika jezi za Stars.

    Ninachoamini iko timu itafikia kiasi ambacho Yanga SC watakipokea. Rais wa Real Madrid Frolentino Perez aliwahi kuwaambia Juventus kuwa hakuna mchezaji asiyeuzwa baada ya kuulizia upatikanaji wa Zidane. Juve ndio walimjibu Perez kwa dharau kuwa Zidane hauzwi.

    Baada ya wiki moja Perez kutoa kauli ile, Uwanja wa Santiago Bernabeu ulijaa mashabiki waliokuja kutazama utambulisho wa Zidane. Perez alirudi Juve kikubwa na kutoa fedha ambazo Juve walishindwa kuzikataa. Biashara ya Yanga SC na Mzize itaenda kuisha katika namna hii ya Juve, Zidane na Madrid. Ni ngumu kushikilia bomba hadi mwisho.

    Ameandika @abdulmkeyenge1

    Yanga SC
    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleHAYA HAPA MAGAZETI YA LEO TAREHE 11-08-2025
    Next Article SIMBA SC BADO IPO SOKONI

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.