Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » YANGA SC MWENDO WA TUNAPIGA KICHWANI TU
    KITAIFA

    YANGA SC MWENDO WA TUNAPIGA KICHWANI TU

    By AdminSeptember 5, 2025No Comments2 Mins Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    wiki ya wananchi yanga
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    Ali Kamwe, Ofisa Habari wa Yanga SC ameweka wazi kuwa kwa sasa Yanga SC hakuna suala la kupeana matumaini bali ni mwendelezo wa dozi pale ambapo waliishia.

    Ipo wazi kwamba Yanga SC ni mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara kuelekea msimu mpya wa 2025/26. Kwa sasa wana jambo kubwa la Wiki ya Mwananchi ambalo linatarajiwa kufanyika Uwanja wa Mkapa Septemba 12 2025.

    Yanga SC itacheza mchezo wa kirafiki na Klabu ya Bandari ya Kenya na kwa sasa wanaendelea na hamasa kuelekea kilele cha Wiki ya Mwananchi na slogan yao inasema Tunapiga Kichwani Tu.

    “Wanayanga sasa wamevuka level ya kuwa na Slogan za kupeana matumaini, tumekubaliana huu ni msimu wa vitendo na tumegundua watu bado wanataka dozi, kuanzia sasa tunaenda kupiga kichwani tu. Hiyo ndio slogan yetu, Tukipiga kichwani tunacheza na ufahamu. Mwaka huu ni kichwa tu, tumeweka kabisa nyundo kwa ajili ya wale wanaokaza fuvu.

    “Kwa upande wa tiketi, mashabiki wa Yanga SC waendelee kukata tiketi kwa kuwa kila kitu kinakwenda sawa.Kulikuwa na changamoto mwanzo lakini kwa sasa kila sehemu wapo wanaouza tiketi. Na ukiona mwamvuli wenye nembo ya Wiki ya Mwananchi wewe kata tiketi.”

    Katika uzinduzi wa Wiki ya Mwananchi, Septemba 3 2025 Mbagala, mashabiki wengi wa Yanga SC walijitokeza na kulikuwa na burudani kali kinomanoma siku hiyo na sasa zinahesabiwa siku kabla ya tukio lenyewe kukamilika.

    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleSAFU MPYA YA UONGOZI SIMBA SC IPO HIVI
    Next Article CLATOUS CHAMA KUWAPA FURANGA SINGIDA BLACK STARS

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.