Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home ยป Wafungaji Bora Ligi Kuu ya NBC Tanzania 2025/2026
    KITAIFA

    Wafungaji Bora Ligi Kuu ya NBC Tanzania 2025/2026

    By AdminFebruary 26, 2026No Comments4 Mins Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    Wafungaji Bora Ligi Kuu ya NBC Tanzania 2025/2026 | Vinara wa Magoli NBC Premier league 2025-26 | Wafungaji Bora Ligi Kuu ya NBC 2025/2026 | Wafungaji bora wa Ligi kuu Tanzania bara | Wafungaji NBC 2025/26

    Wafungaji Bora Ligi Kuu ya NBC Tanzania 2025/2026

    Ligi Kuu ya Tanzania Bara, almaarufu kama NBC Premier League, imeanza kwa kishindo msimu wa 2025/2026. Michuano hii inashirikisha timu 16 bora kutoka maeneo mbalimbali ya Tanzania, zikishindana kwa ari na nguvu ili kufukuzia heshima ya kuwa mabingwa. Yanga SC, mabingwa watetezi, wanaingia msimu huu wakiwa na jukumu la kulinda taji lao, huku nyota wao Clement Mzize akitazamiwa kuendeleza moto wa mabao baada ya msimu uliopita kuibuka kinara wa wafungaji Yanga kwa mabao 13.

    Kwa mujibu wa ratiba iliyotangazwa na Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), pazia la msimu huu limefunguliwa rasmi tarehe 17 Septemba 2025 kwa michezo miwili ya awali: KMC dhidi ya Dodoma Jiji kwenye uwanja wa KMC Complex, Dar es Salaam, na Coastal Union dhidi ya Tanzania Prisons katika uwanja wa Mkwakwani, Tanga. Ratiba pia imeweka bayana kwamba msimu utamalizika 23 Mei 2026, ili kutoa nafasi kwa wachezaji wa Taifa Stars na wachezaji wengine wa Afrika wanaoshiriki Kombe la Dunia 2026 kujiandaa ipasavyo.

    Zaidi ya ubingwa, kipengele kingine kinachoongeza msisimko wa ligi ni mbio za kumsaka Mfungaji Bora wa NBC Premier League 2025/2026. Kila msimu, wachezaji wenye vipaji vya hali ya juu hujitahidi kuonyesha makali yao mbele ya goli ili kutwaa Kiatu cha Dhahabu, tuzo inayotolewa kwa mfungaji mwenye mabao mengi zaidi. Msimu huu unatarajiwa kuwa na ushindani mkali zaidi, kwani nyota chipukizi na wale wenye uzoefu wote wanapambana kutikisa nyavu na kujipatia nafasi katika historia ya soka la Tanzania.

    Orodha ya Wafungaji Bora Ligi Kuu ya NBC Tanzania 2025/2026

    Hadi sasa, katika michezo ya awali ya ligi, wachezaji kadhaa tayari wameanza kujihakikishia nafasi kwenye mbio za kiatu cha dhahabu. Hawa ndiyo wafungaji bora wa NBC Premier League 2025/2026 waliokwisha fumania nyavu:

    Nafasi Mchezaji Klabu Magoli
    1 Fabrice Wa Ngoy Namungo 7
    2 Saleh Karabaka JKT Tanzania 6
    3 William Edgar Dodoma Jiji 5
    4 Iddy Selemani Azam 5
    5 Paul Peter JKT Tanzania 5
    6 Mathew Tegisi Pamba Jiji 4
    7 Prince Dube Young Africans 4
    8 Selemani Mwalimu Simba 4
    9 Laurindo Dilson Depu Young Africans 4
    10 Jonathan Sowah Simba 3
    11 Feisal Salum Azam 3
    12 Valentino Mashaka JKT Tanzania 3
    13 Pacome Zouzoua Young Africans 3
    14 Darueshi Saliboko KMC 3
    15 Cyprian Kipenye Namungo 3
    16 Peter Lwasa Pamba Jiji 3
    17 Magata Charles Mtibwa Sugar 3
    18 Rushine De Reuck Simba 3
    19 Shiza Kichuya Coastal Union 3
    20 George Mpole Tanzania Prisons 3
    21 Maxi Nzengeli Young Africans 2
    22 Cleophace Mkandala Coastal Union 2
    23 Oscar Mwajanga Tanzania Prisons 2
    24 Yasini Mgaza Dodoma Jiji 2
    25 ANDY BOYELI Young Africans 2
    26 Maabad Maulid Coastal Union 2
    27 Athuman Makambo Coastal Union 2
    28 Shassir Nahimana Pamba Jiji 2
    29 Eliud Ambokile Mbeya City 2
    30 Ismail Mhesa Mtibwa Sugar 2
    31 Clatous Chama Simba 2
    32 Mundhir Vuai Mashujaa 2
    33 Jafari Kibaya Mashujaa 2
    34 Bakari Selemani Coastal Union 2
    35 Iddi Kipagwile Dodoma Jiji 2
    36 Vitalisy Mayanga Mbeya City 2
    37 Kelvin Nashon Pamba Jiji 2
    38 Adilly Buha Mbeya City 2
    39 Mudathir Yahya Young Africans 2
    40 Libasse Gueye Simba 2

    Kwa kuzingatia kiwango kilichoonyeshwa kwenye michezo ya mwanzo, wazi kuwa ushindani utakuwa mkali zaidi kadri msimu unavyosonga. Vilabu vikubwa kama Young Africans, Simba SC, na Azam FC vitategemewa kuibua nyota wanaoweza kuongeza kasi ya mabao, huku wachezaji kutoka timu za kati na chini wakionyesha dhamira ya kushindana bila woga.

    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleYanga Yatuma Salamu Msimbazi Baada ya Ushindi wa 5-0 Dhidi ya JKT Tanzania
    Next Article AUDIO | Angel Benard – NIMEONA (Live) MP3 DOWNLOAD

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.