Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » VITA YA KUSAKA POINT TATU MECHI YA SIMBA VS JKT TANZANIA NI BALAA
    KITAIFA

    VITA YA KUSAKA POINT TATU MECHI YA SIMBA VS JKT TANZANIA NI BALAA

    By AdminNovember 7, 2025No Comments2 Mins Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    Mchezo mkali wa Ligi Kuu NBC msimu wa 2025/26 unaendelea kupamba moto, ambapo timu ya JKT Tanzania inatarajiwa kuikaribisha Simba SC katika Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo mnamo Novemba 8, 2025.

    Katika mchezo wa mwisho kukutana msimu uliopita, Simba SC ilivuna pointi tatu ugenini baada ya kushinda kwa bao 1-0, bao lililofungwa na Fabrince Ngoma ambaye kwa sasa hayupo kwenye kikosi cha Simba msimu huu. Hivyo, mchezo wa safari hii unatarajiwa kuwa na upeo tofauti kutokana na mabadiliko ya vikosi na mbinu za makocha.

    Akizungumza kuelekea mchezo huo, Kocha Msaidizi wa Simba SC, Seleman Matola, amesema maandalizi wameyafanya kikamilifu na wanatambua ugumu wa pambano hilo kutokana na uimara wa wapinzani wao.

    “Tunatambua kwamba mchezo utakuwa mgumu lakini tupo tayari. Kikubwa ni kuona tunapata pointi tatu muhimu,” amesema Matola.

    Kwa upande wa mwenendo wa ligi, JKT Tanzania hadi sasa ipo nafasi ya tano ikiwa na pointi 7 baada ya mechi tano, ikishinda mchezo mmoja na kupata sare katika mechi nne. Hali hii inaonesha kuwa ni timu inayocheza kwa nidhamu na ugumu wa kukubali kupoteza.

    Simba SC inashika nafasi ya saba ikiwa na pointi 6 baada ya mechi mbili, ambazo zote ilicheza nyumbani na kuibuka na ushindi. Mchezo huu utakuwa wao wa kwanza ugenini msimu huu, jambo linaloongeza hamasa ya kuona namna watakavyojimudu mbali na nyumbani.

    Mashabiki wa soka nchini wanatarajia mchezo wenye kasi, ushindani na mbinu, hasa katika eneo la kiungo ambapo timu zote zimeonesha uimara.

    JKT Tanzania Simba SC
    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleMikoa Yote Matokeo Ya Darasa La Saba 2025/2026 – NECTA Standard Seven Results (PSLE)
    Next Article TUZO ZA CAF RASMI KUTOLEWA MOROCCO

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.