Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » TUMEFUATA SHERIA, HAKUNA KURUKA HATUA. MANGUNGU
    KITAIFA

    TUMEFUATA SHERIA, HAKUNA KURUKA HATUA. MANGUNGU

    By AdminFebruary 19, 2026No Comments1 Min Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    MWENYEKITI wa Simba, Muhtaza Mangungu, amesema uongozi wa klabu hiyo umepokea rasmi maboresho ya Katiba kutoka Serikalini na tayari umeanza kuyafanyia kazi kwa kuzingatia taratibu na sheria za nchi.

    Kauli hiyo imekuja kufuatia hatua ya Msajili wa Vyama vya Michezo kupitia Baraza la Michezo la Taifa (BMT) kuikabidhi Simba Katiba yao iliyofanyiwa marekebisho, huku wakisisitiza klabu kuendelea na mchakato huo kama ilivyoelekezwa.

    Mangungu ameeleza kuwa uongozi umepokea maelekezo hayo na unahitaji muda wa kuyapitia na kuyatekeleza kwa umakini, ili kuhakikisha kila kipengele kinafanyiwa kazi kwa mujibu wa masharti yaliyowekwa ndani ya Katiba hiyo pamoja na miongozo ya kisheria.

    Amesisitiza kuwa mchakato wa mabadiliko ndani ya klabu si jambo dogo, kwani unagusa mamlaka zaidi ya moja za Serikali, hali inayohitaji umakini na uratibu wa kina.

    “Kuna eneo linalosimamiwa na Wizara ya Michezo, kuna eneo linalosimamiwa na Wizara ya Katiba na Sheria, pia  linalosimamiwa na Wizara ya Viwanda na Biashara,” amesema Mangungu, akibainisha kuwa kila hatua lazima izingatie matakwa ya kisheria.

    Ameongeza kuwa mchakato huo ulianza muda mrefu, hivyo utekelezaji wake unahitaji subira na kufuata taratibu zote za kisheria ili kuhakikisha mageuzi hayo yanafanyika kwa usahihi na kwa manufaa ya klabu pamoja na wanachama wake.

    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleTFF Yafungua Zabuni ya Haki za Kipekee za Ubashiri Dabi ya Kariakoo
    Next Article Barcelona Yatakiwa Kulipa Pauni 26M Kumng’oa Rashford Manchester United

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.