Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » PEDRO KILA KITU REHANI, YANGA KUPIGANIA ROBO FAINALI
    KITAIFA

    PEDRO KILA KITU REHANI, YANGA KUPIGANIA ROBO FAINALI

    By AdminFebruary 11, 2026No Comments2 Mins Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    KOCHA wa Yanga, Pedro Goncalves, ameweka wazi kuwa kikosi chake hakina jambo jingine kichwani kwa sasa zaidi ya kushinda na kutinga robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

    Kwa mujibu wa kocha huyo, malengo ni moja tu Jumapili hii  kuibuka na ushindi dhidi ya JS Kabylie na kusonga mbele katika hatua inayofuata ya michuano hiyo mikubwa barani Afrika.

    Yanga watakuwa wenyeji katika mchezo huo wa mwisho wa hatua ya makundi utakaopigwa Jumapili,  Uwanja wa New Amaan Complex, visiwani Zanzibar.

    Faida ya kucheza nyumbani inatajwa kuwa moja ya silaha muhimu kwa Wananchi, huku wakitarajia sapoti kubwa kutoka kwa mashabiki wao watakaofurika kuishangilia timu yao.

    Hata hivyo, hesabu za kufuzu bado zinaonekana kuwa ngumu. Matokeo ya mchezo mwingine kati ya Al Ahly na FAR Rabat yanaweza kuwa na ushawishi mkubwa katika hatima ya Yanga.

    Endapo FAR Rabat itapata ushindi, hali hiyo inaweza kuifanya Yanga kuwa katika wakati mgumu zaidi wa kusonga mbele, jambo linalowalazimu kupambana kwa nguvu zote bila kutegemea msaada wa matokeo ya pembeni.

    Wakati mashabiki wakihangaika kupiga mahesabu na kuombea matokeo mazuri kutoka katika mchezo wa Al Ahly dhidi ya FAR Rabat, benchi la ufundi la Yanga limeamua kuhamishia nguvu zote uwanjani.

    Pedro amesisitiza kuwa timu yake haitakiwi kuyumba kisaikolojia kwa kuangalia kinachoendelea kwingine, bali ijikite katika kutimiza wajibu wake wa kushinda.

    Kwa mujibu wa taarifa za ndani ya kambi ya Yanga, maandalizi yamekuwa makini na yenye umakini mkubwa, huku wachezaji wakionyesha ari na morali ya hali ya juu.

    Pedro ameandaa mkakati maalum wa kiufundi na kisaikolojia ili kuhakikisha kikosi chake kinacheza kwa nidhamu, umakini na ufanisi mkubwa mbele ya lango.

    Sasa macho na masikio ya Wananchi yote yataelekezwa New Amaan Complex, wakiamini kuwa chini ya Pedro, Yanga inaweza kuandika historia nyingine kwa kutinga robo fainali.

    Kila kitu kitaamuliwa ndani ya dakika 90, ambapo ushindi pekee ndio tiketi ya ndoto za kuendelea na safari ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleMO DEWJI AHOJI MAGEUZI SIMBA, GUMZO MTANDAONI
    Next Article KIBU DENIS NDIO BASI TENA SIMBA, AAGA RASMI

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.