Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » ONYO LA MAPEMA, YANGA YAREJEA KILELENI KWA KISHINDO
    KITAIFA

    ONYO LA MAPEMA, YANGA YAREJEA KILELENI KWA KISHINDO

    By AdminFebruary 26, 2026No Comments1 Min Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    KLABU  ya Yanga imerejea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara baada ya kuibuka na ushindi mnono wa mabao 5-0 dhidi ya JKT Tanzania katika mchezo uliopigwa kwa ushindani mkubwa.l katika dimba la KMC Complex uliopo Mwenge Dar es Salaam.

    Katika pambano hilo, Yanga ilionyesha ubora mkubwa kuanzia dakika za mwanzo hadi mwisho wa mchezo, ikitawala umiliki wa mpira na kutengeneza nafasi nyingi za mabao.

    Ushindi huo umeipa timu hiyo morali kubwa kuelekea michezo ijayo, hususan Kariakoo Derby inayosubiriwa kwa hamu na mashabiki.

    Mabao ya Yanga yalifungwa na Mohamed Hussein, Laurindo Dilson ‘Depu’, Mudathir Yahya, Prince Dube na Sheikhan Khamis, kila mmoja akichangia kwa namna yake kuifanya timu hiyo iondoke na alama zote tatu muhimu.

    Kwa matokeo hayo, Yanga imefikisha pointi 28 na kurejea kileleni mwa msimamo wa ligi ikiwa na pointi sawa na JKT Tanzania waliopo nafasi ya pili. Hata hivyo, Yanga inaongoza kutokana na ubora wa tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa.

    Ushindi huo si tu umeimarisha nafasi yao juu ya msimamo, bali pia umetuma salamu nzito kwa wapinzani wao kabla ya Kariakoo Derby, huku kikosi hicho kikionekana kuwa katika kiwango bora na tayari kwa mapambano makubwa yanayofuata.

    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleKikosi cha Simba vs Dodoma Jiji Leo 25/02/2026
    Next Article Yanga Yatuma Salamu Msimbazi Baada ya Ushindi wa 5-0 Dhidi ya JKT Tanzania

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.