Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » NYOTA WATATU WAMTIBULIA LAIZER FOUNTAIN GATE
    KITAIFA

    NYOTA WATATU WAMTIBULIA LAIZER FOUNTAIN GATE

    By AdminFebruary 23, 2026No Comments2 Mins Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    KOCHA Mkuu wa Fountain Gate, Mohamed Ismail ‘Laizer’, amesema kuwakosa wachezaji watatu waliofikia makubaliano ya kutua ndani ya kikosi hicho katika dirisha dogo la Januari 2026, ni pigo kubwa kwake, kutokana na matarajio aliyokuwa nayo.

    Nyota walioshindwa kujiunga na timu hiyo katika dirisha dogo ni, mshambuliaji wa Mbeya Kwanza, Boniface Mwanjonde, winga, Tariq Mohamed Mkonga aliyetoka JKU SC ya visiwani Zanzibar na kiungo, Saleh Masoud Abdallah ‘Tumbo’ aliyetokea Pamba Jiji.

    Wachezaji wote watatu, walifikia makubaliano ya kujiunga na timu hiyo na tayari walisaini mikataba ya miaka miwili kwa kila mmoja wao, ingawa dili hizo zilikufa mwishoni, baada ya Fountain Gate kupokea barua rasmi ya kufungiwa kusajili.

    Akizungumza na Soka la Bongo, Laizer, amesema alikuwa na matarajio makubwa kwa wachezaji wote watatu ili wakaongeze nguvu kikosi hicho, lakini dili hizo zilishindikana, jambo lililowavunja moyo benchi lao nzima la ufundi.

    “Kwa sasa tunaendelea kupambana na wachezaji waliopo, kiukweli tulitarajia mambo makubwa kwa sababu ya viwango ambavyo walikuwa navyo katika timu walizotoka, mwenendo wetu sio mzuri, hivyo, tunapaswa kuzidisha juhudi sana,” amesema Laizer.

    Fountain ndio timu ambayo tangu mwaka 2026, umeanza haijaonja ladha ya ushindi katika mechi za Ligi Kuu, tangu mara ya mwisho kikosi hicho kilipoifunga Tanzania Prisons bao 1-0, kwenye Uwanja wa Tanzanite Kwaraa, Babati, Novemba 26, 2025.

    Timu hii iliyohamishia makazi yake kwa sasa jijini Arusha ikiutumia Uwanja wa Sheikh Amri Abeid tangu Nov26 imecheza mechi tano imechapwa tatu na kutoka sare mbili.

    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleSingida Black Stars yaituliza Mtibwa Sugar
    Next Article Mayele Aendelea Kupambana na Ukame wa Mabao Pyramids FC

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.