Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home ยป NASIMAMA NA SIMBA NA AZAM WALIOCHAGUA KUKAA KIMNYA
    KITAIFA

    NASIMAMA NA SIMBA NA AZAM WALIOCHAGUA KUKAA KIMNYA

    By AdminAugust 19, 2025No Comments2 Mins Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    “Nimeona andiko la kaka yangu Jemedari Said kuzihusu Simba SC na Azam FC kutokutoa matokeo yao ya mechi zao za kirafiki walizocheza.

    Azam FC walifungwa 2-1 na JKT Tanzania pale Arusha. Simba SC wakafungwa 4-3 na Enpipp pale Misri. Kwangu ni tofauti kidogo.

    Nasimama na Azam FC na Simba SC waliochagua kukaa kimya na taarifa za matokeo ya mechi zao. Kuna kitu kinaitwa mechi za Indoor. Hizi ni mechi ambazo hazina mashabiki. Hazitakiwi kutoka nje ndio maana zikaitwa Indoor.

    Makocha wanapenda kuzitumia mechi hizi kwa ajili ya kutazama mbinu zao zinafanyaje kazi. Timu zetu huwa zinacheza sana mechi zenye sura hii.

    Simba ambao walifungwa juzi, walicheza mechi nyingine na walishinda, lakini hawajapost matokeo ya mechi katika ukurasa wao na hata mtu mmoja aliyehoji.

    Hata waliotoa taarifa ya mechi ile ambayo Simba SC walishinda walipata shida kupata matokeo. Lakini hi haikuonekana kama ni shida.

    Kilionekana kitu cha kawaida tu. Kama Simba wangetoa matokeo ya mechi ile waliyoshinda, kisha hawajapost matokeo ya mechi ya juzi, ingeleta shida kwa wapenzi wao na moja kwa moja tungesema wanachagua taarifa za kuzitoa.

    Lakini walivyoshinda hawajatoa matokeo. Kwanini tuhoji walivyofungwa? Mimi naamini hizi ni mechi ambazo zipo sana na zinachezwa sana pale Avic Town. Bunju Arena. Chamazi. KMC Complex zinachezwa sana, tena kila siku au nyingine asubuhi na nyingine jioni. Ni mechi za kawaida mno. Ni kawaida sana.

    Binafsi nimewahi kushuhudia mechi zenye sura hii nyingi tu zilizokosa idadi. Tena nimetazama mechi za Simba SC na Yanga SC matokeo yake yanabaki ndani pale pale” Ameenda Mkunga

    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleRAIS WA FIFA AMPONGEZA KARIA KWA KUREJEA TENA MADARAKANI
    Next Article PITIA MAGAZETI YA MICHEZO LEO TAREHE 20 AGOSTI 2025

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.