Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » MANGUNGU: MABADILIKO YA BENCHI LA UFUNDI NDIO YALIIVURUGA SIMBA
    KITAIFA

    MANGUNGU: MABADILIKO YA BENCHI LA UFUNDI NDIO YALIIVURUGA SIMBA

    By AdminFebruary 5, 2026No Comments2 Mins Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    mangungu
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    MWENYEKITI wa Klabu ya Simba, Murtaza Mangungu, amesema mabadiliko ya ghafla katika benchi la ufundi yamechangia kwa kiasi kikubwa kutokuwa na mwanzo mzuri wa msimu huu kwa timu hiyo.

    Mangungu amesema msimu uliopita Simba ilikuwa chini ya kocha mpya, Fadlu Davids, ambaye alihitaji aina maalumu ya wachezaji watakaokwenda sambamba na falsafa yake ya soka, jambo lililowasaidia kumaliza msimu katika nafasi ya pili na kufika fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

    Ameeleza kuwa walipoanza msimu huu, uongozi uliingia sokoni kusajili wachezaji kulingana na mapendekezo ya kocha huyo, lakini ujio wa ofa kubwa kwa Davids uliwalazimu kumuacha aondoke, hali iliyovuruga mipango yao mapema.

    “Wakati tunaanza msimu na kusajili wachezaji aliowapendekeza, ikaja ofa kubwa kwake na hatukuwa na budi kumzuia. Hilo lilituvuruga sana kwa sababu tulilazimika kuingia sokoni tena kutafuta kocha mwingine,” amesema Mangungu.

    Ameongeza kuwa Simba ilifanikiwa kumpata Steve Barker, ambaye naye amekuja na falsafa yake ya uchezaji, hivyo kulikuwa na ulazima wa kufanya usajili mwingine wa wachezaji watakaosaidia timu kufikia malengo yake.

    Mangungu amesema ujio wa kocha mpya katikati ya mashindano, pamoja na usajili wa wachezaji wapya, bado ni changamoto kwa timu kutokana na kukosekana kwa muunganiko wa pamoja.

    Amefafanua kuwa mafanikio ya timu si juhudi zake peke yake bali ni matokeo ya ushirikiano wa viongozi wengine, hata hivyo lawama nyingi hutupwa kwake pale timu inapofanya vibaya.

    “Jambo ninalokubaliana nalo ni waache wapewe sifa wanaowapenda, lakini lawama zije kwangu. Mimi siwezi kufanya timu ifanye vibaya kwa makusudi, kwa sababu tumeunda bodi na menejimenti yenye uwezo wa kufanya kazi na benchi la ufundi au wachezaji,” amesema.

    Ameongeza kuwa kulingana na mgawanyo wa majukumu, yeye binafsi hana nafasi ya kukutana moja kwa moja na wachezaji, bali bodi hukaa na kuwasilisha maelekezo kwa menejimenti ili yawafikie wachezaji.

    Mangungu amesema kelele na vurugu zinazoshuhudiwa hazichochewi na mashabiki au wanachama wa kweli wa Simba, bali ni watu wachache walioundwa kwa ajili ya propaganda na kuiondoa klabu hiyo kwenye mstari wake.

    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleSALUM MAYANGA AKALIA KUTI KAVU MASHUJAA
    Next Article MMILIKI WA MBEYA KWANZA APIGA MKWARA HUU MZITO

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.