Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » MAAMUZI MAGUMU KUHUSU UTATA WA BAO LA SOWAH YATAJWA
    KITAIFA

    MAAMUZI MAGUMU KUHUSU UTATA WA BAO LA SOWAH YATAJWA

    By AdminNovember 10, 2025No Comments1 Min Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    sowah
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    Jonathan Sowah, mshambuliaji wa Simba SC, amezua mjadala baada ya bao lake dhidi ya JKT Tanzania kutajwa kuwa lina utata, ikidaiwa huenda alikuwa ameotea wakati akifunga.

    Bao hilo lilifungwa Novemba 8, 2025 kwenye Uwanja wa Meja Isamuhyo, mchezo ambao uliisha kwa JKT Tanzania 1-2 Simba SC.

    Katika mchezo huo uliojaa ushindani, JKT Tanzania walitangulia kupata bao kupitia Edward Songo, kabla ya Simba SC kusawazisha na kuongeza kupitia mabao ya Wilson Nangu aliyefunga kwa kichwa, na Jonathan Sowah aliyepachika bao baada ya kupokea pasi kutoka kwa Morice Abraham.

    Akizungumzia ushindi huo, Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Simba SC alisema wanachotambua ni kwamba walipata ushindi kwenye mchezo mgumu, kwa kutumia mbinu sahihi na silaha walizokuwa nazo ndani ya kikosi.

    “Tulijua mchezo ungekuwa mgumu, ndio maana mabao yalifungwa kwa juhudi na mbinu maalum. Unaona jinsi pasi zinavyopenya katikati ya mabeki, wanaishia kujikuta wanashindwa kuchukua maamuzi haraka kwa sababu ni pasi za hatari.

    “Tulitumie silaha tulizokuwa nazo, ukiwaangalia mlinda mlango Yakoub na beki Nangu, hawa ni wachezaji walioonyesha ubora mkubwa. Tunamshukuru Mungu kwa kutupa pointi tatu,” alisema.

    Simba SC
    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleHAYA HAPA MAGAZETI YA LEO NOVEMBA 10, 2025
    Next Article MAKUBWA!! UWEPO WA ABRAHAM MORICE WAZUA BALAA HILI SIMBA

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.