Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » LOEMBA, CHAMA KUWA PAMOJA LIGI KUU HAITAELEWEKA
    KITAIFA

    LOEMBA, CHAMA KUWA PAMOJA LIGI KUU HAITAELEWEKA

    By AdminFebruary 10, 2026No Comments2 Mins Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    MENEJA Idara ya Habari na Mawasiliano ya Simba, Ahmed Ally, ameonya wapinzani wa Ligi Kuu Tanzania Bara kuhusu ubora wa safu ya kiungo wa timu hiyo, akisema kuwa itakuwa changamoto kubwa msimu huu.

    Kauli hiyo inakuja baada ya kiungo mshambuliaji, Iñno Jospin Loemba, kuonyesha kiwango cha juu katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Petro de Luanda ya Angola.

    Ahmed amesema  Loemba, ambaye alijiunga na Simba katika dirisha dogo la usajili, ameanza kuonyesha umuhimu wake katika timu kwa kuungana vyema na Clatous Chama.

    “Loemba anacheza kama namba 8 au 10, lakini ana uwezo mkubwa, mawinga wanapaswa kujua jinsi ya kumtumia vyema,” amesema Ahmed.

    Katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Petro de Luanda, Loemba alionyesha kiwango bora licha ya kuingia akitokea benchi, akitoa pasi ya bao la kusawazisha lililofungwa na Anicet Oura.

    Hii ilikuwa mechi yake ya kwanza tangu kujiunga na Simba, lakini alionyesha ufanisi mkubwa, na Ahmed alisisitiza kuwa uhusiano wake mzuri na Chama utakuwa na athari kubwa kwenye ligi.

    “Ikiwa Loemba atapata uelewano mzuri zaidi na Chama, basi wapinzani wa Ligi Kuu Tanzania Bara watapata changamoto kubwa. Akielewana vizuri na Chama, watasema kwa lugha yao.” amesema na kuongeza kuwa;

    Hii ni onyo kwa wapinzani wa Simba kwamba, pamoja na hali ya ushindani, safu ya kiungo ya timu hiyo itakuwa ni silaha muhimu katika mapambano ya ligi kuu.

    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleSIMBA WATIKISWA, YANGA WAPANGIA ROBO FAINALI
    Next Article LIVERPOOL ILIMCHELEWESHA SANA LUIS DIAZ

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.