Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » KUELEKEA DABI YA KARIAKOO……YANGA MAPEMAAAA TU…..SHILINGI IKO JANGWANI KITAMBO
    KITAIFA

    KUELEKEA DABI YA KARIAKOO……YANGA MAPEMAAAA TU…..SHILINGI IKO JANGWANI KITAMBO

    By AdminFebruary 28, 2026No Comments2 Mins Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    KIPUTE cha watani wa jadi kati ya Yanga na Simba kinatarajiwa kupigwa Jumapili, Machi 01, 2026, kwenye Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar kuanzia saa 2:15 usiku.

    Mchezo huo unakuja katika kipindi ambacho Yanga wanaingia wakiwa na rekodi bora dhidi ya watani wao, baada ya kushinda mechi sita mfululizo za mwisho za Dabi ya Kariakoo.

    Katika michezo hiyo sita, Yanga waliibuka na ushindi wa mabao 5-1, 2-1, 1-0, 1-0, 2-0 na 1-0 dhidi ya Simba, wakionesha ubabe wa wazi katika miaka ya karibuni.

    Takwimu hizo zinaweka presha kubwa kwa Simba ambao wataingia dimbani wakihitaji kuvunja mwendelezo huo na kurejesha heshima yao mbele ya mashabiki.

    Waamuzi Watajwa
    Kamati ya waamuzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imemtaja Nassoro Mwinchui kuwa mwamuzi wa kati katika pambano hilo, akisaidiwa na Kassim Mpanga na Hamdan Said, huku Ramadhani Kayoko akiwa mwamuzi wa akiba.

    Rekodi zingali Hai
    Historia ya dabi hiyo iliyoanza mwaka 1965 imebeba matukio mengi makubwa ambayo baadhi yake hayajawahi kuvunjwa hadi sasa.

    Miongoni mwa rekodi hizo ni ya Abdallah Kibadeni wa Simba aliyefunga mabao matatu katika dabi ya mwaka 1977, akiwa mchezaji pekee kufunga ‘hat-trick’ katika historia ya pambano hilo.

    Katika mechi hiyo, Simba waliibuka na ushindi wa mabao 6-0, huku mabao mengine yakifungwa na Jumanne Hassan aliyefunga mawili na bao moja likiwa la kujifunga la beki wa Yanga, Seleman Sanga.

    Aidha, mwaka 2013 katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, Yanga waliwahi kuongoza kwa mabao 3-0 kabla ya Simba kusawazisha na kufanya matokeo kuwa 3-3 katika mchezo uliovuta hisia za mashabiki wengi.

    Pia mwaka 1996 kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, timu hizo zilitoka sare ya mabao 4-4 katika moja ya mechi zenye mabao mengi zaidi katika historia ya dabi hiyo.

    Dakika 90 Za Maamuzi
    Licha ya rekodi na takwimu, dabi ya Kariakoo imekuwa ikijulikana kwa matokeo yasiyotabirika.

    Yanga wataingia wakisaka kuendeleza ubabe wao wa hivi karibuni, huku Simba wakisaka ushindi wa kurejesha matumaini na kuvunja mwiko wa kupoteza mechi sita mfululizo. Itakuwa ni presha kwa wekundu hao ambao muda mrefu hawajaifunga Yanga.

    Mashabiki sasa wanasubiri kuona nani atatabasamu baada ya dakika 90 ndani ya Amaan Complex.

    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleHii Hapa Orodha ya Waamuzi wa Dabi ya Kariakoo 2026
    Next Article Ally Kamwe: Kariakoo Dabi Ilijawa na Ushirikina Usio wa Lazima

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.