Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » KIUNGO KAGERA SUGAR, JKT TANZANIA MSHAMBULIAJI KUREJESHA KWA JAMII, MKUDE NDANI
    KITAIFA

    KIUNGO KAGERA SUGAR, JKT TANZANIA MSHAMBULIAJI KUREJESHA KWA JAMII, MKUDE NDANI

    By AdminJuly 2, 2025No Comments2 Mins Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Mkudeee
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    KATIKA kurejesha kwa jamii wachezaji, Nassor Kapama ambaye ni kiungo wa Kagera Sugar pamoja na mshambuliaji wa JKT Tanzania, Mohammed Bakari ‘Muddy Beka’ Julai 12, mwaka huu wanatarajia kucheza mechi ya hisani ikiwa na lengo maalum la kusaidia watu wasiojiweza.

    Mechi hiyo imeeandaliwa maalum na nyota hao ambao wanashiriki Ligi Kuu Bara ambapo itafanyika katika Uwanja wa Shule ya Msingi Kigamboni, Dar huku kiasi chote ambacho kitapatikana katika mechi hiyo kitatolewa kwa wahitaji.

    Muandaaji wa mchezo huo, Kapama amesema, kuwa maandalizi ya mchezo huo hadi sasa yanaendelea ambapo lengo kubwa la kufanya hivyo ni kutaka kusaidia wanajamii wa eneo hilo.

    “Hadi sasa kila kitu kinaendelea vizuri kuhusiana na mchezo huu ambao lengo kubwa ni kurudisha kwa jamii ambayo tunakaa nayo lakini pia kutoa kile kidogo ambacho tunacho.

    “Fedha ambazo zitapatikana katika mchezo huu basi zitaenda kwa kundi hilo ambapo tunakaribisha watu na kampuni kuja kudhamini mchezo wetu huu ambao tunatarajia kutakuwa na mastaa mbalimbali wa ligi kuu.

    “Kwenye mechi yetu hii kutakuwa na timu ya Kapama na Timu ya Muddy Beka na baadhi ya mastaa ambao watakuwa sehemu ya mchezo huu ni Mkude (Jonas), Erasto Nyoni, Hassan Dilunga, Joash Onyango, Abdultwalib Mshery, Hussein Kazi, Abal Kassim na wengine zaidi tutawatambulisha kwa kila siku zinavyokwenda,” alisema Kapama.

    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleBEKI YANGA SC MKATABA WAKE UMEKWISHA, ATAJA ATAKAPOSAINI
    Next Article ALI KAMWE, ASHANGAZWA NA MAUNO YA BONGE LA DADA

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.