Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home ยป KISA KUMPIGA MWAMUZI, ‘KIHIMBWA’ ASIMAMISHWA FOUNTAIN GATE FC
    KITAIFA

    KISA KUMPIGA MWAMUZI, ‘KIHIMBWA’ ASIMAMISHWA FOUNTAIN GATE FC

    By AdminJune 14, 2025No Comments2 Mins Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Fountain Gate FC
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    Uongozi wa timu ya Fountain Gate FC yenye makazi yake Babati mkoani Manyara imemsimamisha nyota wao Salum Kihimbwa kwa muda usiojulikana kutokana na utovu wa nidhamu.

    Kihimbwa msimu huu amekuwa na kiwango bora katika Ligi Kuu Bara, ambapo amehusika katika mabao tisa ndani ya timu hiyo, akifunga nne na kutoa pasi za mabao matano.

    Amesimamishwa kwa muda usiojulikana baada ya kumpiga mwamuzi katika mchezo wa kirafiki ambao Fountain Gate ilicheza dhidi ya Wapolo FC katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid uliopo jijini Arusha.

    Katika mchezo huo wa kirafiki Kihimbwa alionyeshwa kadi nyekundu baada ya kumchezea madhambi mchezaji wa Wapolo FC ambapo mchezaji huyo alionekana kupinga maamuzi ya mwamuzi wa kati na kumpiga ngumi ya uso. Wakati huo Fountain Gate ilikuwa inaongoza kwa magoli 2-1.

    Mratibu wa Fountain Gate FC, Wendo Makau ameiambia Mwanaspoti kuwa wamefikia uamuzi wa kumsimamisha mchezo huyo kwa muda usiojulikana ili kulinda taswira ya timu yao ambayo wameijenga muda mrefu.

    “Kwetu sisi kama Fountain Gate mchezaji asipokuwa na nidhamu hata awe na kiwango kizuri vipi tunamtoa kwa hiyo Kihimbwa anaweza kurudi au asirudi,” amesema Makau.

    Ametumia fursa hiyo kuwataka wachezaji wote kuhakikisha wanakuwa na nidhamu ili kulinda taswira ya timu huku wakitambua kuwa mpira ni ajira na ajira yoyote ile inahitaji nidhamu ya hali ya juu.

    Fountain Gate FC imeweka kambi jijini Arusha kwa ajili ya maandalizi kuelekea mechi mbili za Ligi Kuu Bara ambazo zimesalia kwa upande wao dhidi ya Coastal Union FC na Azam FC ambazo ni muhimu kushinda ili kujitengenezea mazingira mazuri ya kukwepa kucheza hatua ya mtoano (play off).

    Fountain Gate FC
    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleTFF YATANGAZA UCHAGUZI MKUU AGOSTI 16, 2025 JIJINI TANGA
    Next Article YANGA SC YAZITAKA TATU ZA TANZANIA PRISONS

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.