Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » KINACHOENDELEA KAMBINI KWA TAIFA STARS, MISRI
    KITAIFA

    KINACHOENDELEA KAMBINI KWA TAIFA STARS, MISRI

    By AdminJuly 12, 2025No Comments2 Mins Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Taifa Stars
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    KIKOSI cha timu ya soka ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ kinaendelea na mazoezi kwenye kambi yake nchini Misri kujiandaa na Fainali za Ubingwa wa Mataifa ya Afrika (CHAN) zinazotarajiwa kuanza Agosti 2 hadi 30, mwaka huu.
    Taifa Stars imekuwa ikifanya mazoezi viwanja vya Mercure Jijini Ismailia, Misri tangu iwasili Julai 8 kujiandaa na fainali hizo zinazoandaliwa kwa pamoja na Tanzania na nchi jirani za Kenya na Uganda.

    Kikosi kipo chini ya Kocha Mkuu, Hemed Suleiman Ali ‘Morocco’ anayesaidiwa na wazawa wenzake, Juma Ramadhani Mgunda ‘Pep Guardiola Mnene’ na Jamhuri Mussa Kihwelo ‘Julio’ na kinaundwa na wachezaji 27 kutoka klabu tofauti nchini.

    Hao ni pamoja na makipa Aishi Salum Manula ‘Air Manula’ wa Simba SC atakayekuwa pamoja na Hussein Masalanga wa Singida Black Stars na Yakoub Suleiman Ali wa JKT Tanzania.

    Mabeki ni Shomari Kapombe (Simba SC), Lusajo Mwaikenda (Azam FC), Mohamed Hussein (Simba SC), Pascal Msindo (Azam FC), Ibrahim Hamad ‘Bacca’ (Yanga SC), Dickson Job (Yanga SC), Wilson Nangu (JKT Tanzania). Abdurazak Mohamed (Simba SC), Vedastus Masinde (TMA Stars) na Lameck Lawi (Coastal Union).

    Viungo wa katikati ni Ahmed Pipino (KMC), Mudathir Yahya (Yanga SC) na Yusuph Kagoma (Simba SC) — wakati viungo washambuliaji ni Nassor Saadun (Azam FC), Iddi Suleiman ‘Nado’ (Azam FC) na Feisal Salum (Azam FC).
    Wengine ni Kibu Dennis (Simba SC), Jammy Simba (KMC), Sabri Kondo (Coastal Union), Shekhan Khamis (Yanga SC) na Abdul Suleiman ‘Sopu’ (Azam FC), wakati washambuliaji ni Clement Mzize (Yanga SC), Mishamo Michael (Ken Gold) na Ibrahim Hamad Hilika (Tabora United).

    Taifa Stars imepangwa Kundi B pamoja na Madagascar, Mauritania, Burkina Faso na Jamhuri ya Afrika ya Kati (CAR), wakati Kundi A kuna Kenya, Morocco, Angola Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Zambia.
    Kundi C linazikutanisha Uganda, Niger, Guinea, Algeria na Afrika Kusini wakati Kundi D kuna Senegal, Kongo, Sudan na Nigeria.

    Taifa Stars
    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleYANGA YAZINDUA KAMPENI YA “TOFALI LA UBINGWA” KWA AJILI YA USAJILI WA WACHEZAJI BORA
    Next Article SIMBA YAMTOA OMARY OMARY KWA MKOPO KWENDA MASHUJAA FC

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.