Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home ยป HERSI: UMRI ULINIFANYA NISIAMINIKE YANGA
    KITAIFA

    HERSI: UMRI ULINIFANYA NISIAMINIKE YANGA

    By AdminOctober 14, 2025No Comments2 Mins Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Hersi
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    Rais wa Klabu ya Yanga, Injinia Hersi Said, amefunguka kuwa wakati anapewa jukumu la kuiongoza klabu hiyo, baadhi ya wanachama na mashabiki hawakuwa na imani naye kutokana na umri wake kuwa mdogo ukilinganisha na viongozi waliowahi kuiongoza timu hiyo hapo awali.

    Akizungumza kuhusu safari yake ndani ya uongozi wa Yanga, Hersi alisema mashaka ya wanachama yalikuwa ya kawaida kwani wengi walikuwa wakijiuliza kama kijana kama yeye angeweza kuhimili presha na majukumu makubwa ya kuiongoza klabu yenye historia na mashabiki wengi kama Yanga SC.

    “Ni kweli kulikuwa na mashaka, na niliyaelewa. Nilikuwa kiongozi kijana zaidi kuliko waliowahi kuongoza Yanga, hivyo ilikuwa rahisi kwa watu kutilia shaka uwezo wangu,” alisema Hersi.

    Hata hivyo, aliongeza kuwa badala ya kuyumbishwa na maneno hayo, aliamua kuyatumia kama motisha ya kufanya kazi kwa bidii na kuonesha kuwa vijana pia wana uwezo mkubwa wa kuongoza na kufanya maamuzi makubwa yenye manufaa kwa klabu.

    Chini ya uongozi wake, Yanga imeendelea kufanya mageuzi makubwa ndani na nje ya uwanja, ikiwemo kuongeza thamani ya kibiashara ya klabu, kufanya vizuri kwenye michuano ya ndani na nje ya nchi, pamoja na kuimarisha mfumo wa usimamizi wa kisasa ndani ya klabu.

    Mashabiki na wadau wa soka sasa wanamtazama Hersi kama mfano wa viongozi vijana wanaoweza kuleta mabadiliko chanya katika michezo nchini.

    Yanga SC
    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleKOMBE LA DUNIA 2034 KUCHEZWA JANUARY 2035
    Next Article UWANJA WA SOKOINE WAFUNGIWA KUCHEZWA MECHI ZA LIGI KUU

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.