Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » ENG. HERSI SAID AENDELEA KUIBEBA SOKA LA AFRIKA KUPITIA ACA
    KITAIFA

    ENG. HERSI SAID AENDELEA KUIBEBA SOKA LA AFRIKA KUPITIA ACA

    By AdminJuly 6, 2025No Comments1 Min Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Hersi
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    Mwaka uliopita, Chama cha Umoja wa Vilabu Afrika (ACA) chini ya uongozi wa Eng. Hersi Said, kilifanikiwa kushawishi CAF kutoa dola 50,000 kwa kila klabu iliyoshiriki Ligi ya Mabingwa Afrika (CAF CL) na Kombe la Shirikisho (CAF CC) katika hatua ya awali.

    Kwa msimu huu mpya, ACA imeendelea kupigania maslahi ya vilabu barani Afrika kwa mafanikio zaidi. Kupitia mazungumzo na ushawishi wao kwa CAF, imeidhinishwa kuwa klabu zitakazoshiriki hatua ya awali ya CAF CL na CAF CC zitalipwa dola 100,000 kila moja kwa ajili ya maandalizi.

    Ikumbukwe, kabla ya uwepo wa ACA, klabu shiriki katika hatua za awali za mashindano hayo hazikuwa zikipewa msaada wowote wa kifedha na CAF.

    Hatua hii imepongezwa na wadau wengi wa soka barani Afrika kama ishara ya kweli ya mapambano ya kuleta usawa na maendeleo ya vilabu vya Afrika vilivyo katika mazingira magumu ya kifedha.

    Kwa mara nyingine tena, Eng. Hersi Said ameendelea kuthibitisha kujitolea kwake kwa dhati katika kuendeleza soka la Afrika na kupigania maslahi ya vilabu.

    “Hersi anazidi kuipambania football ya Afrika.” – @alikamwe

    Yanga SC
    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleALI KAMWE, ASHANGAZWA NA MAUNO YA BONGE LA DADA
    Next Article BERNARD MORRISON ATOA SHUKRANI KWA WALIOSIMAMA NAYE KATIKA SAFARI YA KUPONA MAJERAHA YA GOTI

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.